Wednesday, 21 December 2016

Sababu Kumi (10) Zinazokuzuia Kuanza Biashara

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala mbalimbali zinazowekwa katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio.

Napenda kukupongeza kwa hatua uliyochukua ya kuamua kutembelea mtandao huu kwa ajili ya kuchota maarifa ambayo yatakusaidia katika maisha yako na pia kukushukuru kwa ajili ya kuwashirikisha marafiki wengine waungane nasi kwa ajili ya kuendelea kuboresha maisha yetu.

Katika makala yetu ya leo napenda kukushirikisha sababu kumi (10) ambazo zinatumika kama pazia la kujifichia au kisingizio cha kusababisha watu wasianze kutengeneza biashara zitakazohudumia watu na hatimaye kuwaingizia kipato.

1. Kukosa fedha (mtaji) kwa ajili ya kuanza biashara.

2. Kuwa na idadi kubwa ya ndugu au jamaa wanaokutegemea kwa ajili ya kuwasaidia kwa huduma mbalimbali kama mahitaji muhimu, elimu na kadhalika.

3. Kukosa mawasiliano na watu ambao wataweza kukuunga mkono katika biashara yako.

4. Kukosa uwezo wa kutosheleza wa kuanza , kuendesha na kusimamia biashara yako.

5. Kukosa muda wa kuendesha na kusimamia biashara kutokana na kutingwa na shughuli nyingine.

Soma Makala Hii Inayohusiana : Mambo Matano (05) Yanayosababisha Kushindwa

6. Kukosa mtu sahihi ambaye anaweza kukuongoza hatua kwa hatua katika biashara mpaka uweze kusimama mwenyewe.

7. Umri wako umeshakwenda sana.

8. Uhitaji wa muda mwingi kutoka kuanza biashara mpaka kukua na kuendelea.

9. Kuchukia kushughulika na wafanyakazi ambao unatakiwa kuwasimamia.

10. Hofu ya kuwa na biashara ni hatari (risky).

Rafiki hizi ni baadhi tu ya sababu zinazotumiwa, je ni sababu ipi umeitumia kujitetea kama hoja ya msingi ambayo inakuzuia mpaka sasa kuanza kutengeneza biashara?

Tafadhali nishirikishe maoni yako kwa kutaja sababu ipi ambayo unaona ndiyo kikwazo kikubwa au kunitajia sababu nyingine unazozifahamu, ili tuweze kuzijadili katika makala zijazo.

Rafiki napenda kukuarifu kuwa ikiwa una maswali au mada ambayo ungependa niiandikie makala , unaweza tuma katika anuani yangu luckmoshi@gmail.com

Goodluck Moshi
Mwandishi
StadizaMafanikio

Related Posts:

  • Njia Rahisi Kuzuia Utendaji MbovuKama hali yetu ya hamasa ya kufanya jambo fulani haifanani/haiendani na jambo tunalohitajika kulifanya, moja kwa moja inapelekea kukosa hamasa ya kulitekeleza hilo jambo. Kukosekana kwa hamasa kutapelekea kulihairisha hilo j… Read More
  • Fahamu Haya Kama KiongoziKwa kila unayemuongoza unahusiana naye kwa kulingana na mojawapo kati ya ngazi hizi tano. Ngazi ya chini kabisa ni ngazi ya kwanza na ngazi ya juu kabisa ni ngazi ya tano: 1. Ngazi ya kwanza ambayo tunaanza nayo katika safar… Read More
  • Jenga Mtazamo Huu Unapouliza MaswaliTukio lolote linapotutokea bila kujali ni zuri au baya katika akili kuna mambo matatu huwa yanaendelea: a) Fikra (thoughts) b) Hisia (feelings) c) Hali (circumstances) Bila kujali hali ya tukio mambo hayo 3 ndiyo yanayotuon… Read More
  • Unahitaji Wastani wa Maswali 12 KufanikiwaUnapofanya maamuzi ya kutaka kufanikiwa unahitaji kufanya mabadiliko ya msingi (fundamental change).Ili kufanya mabadiliko unahitaji namna nzuri ya kuelewa sehemu ambayo unatakiwa kuanzia. Sehemu iliyo bora kabisa ya kuanza… Read More
  • Umakini Unaouhitaji Kabla Hujaanza Kufanya LoloteKutegemeana mtu na mtu kuna tofauti kati ya vitu vinavyoleta bugudha wakati unafanya jambo. Mfano kuna mtu hawezi kufanya kazi katika mazingira yenye kelele au wakati redio inazungumza wakati huo huo kuna mwingine anaweza kuf… Read More

2 comments: