Tuesday, 29 November 2016

Shule Mbili (02) Bora Unazopaswa Kuhudhuria Katika Maisha

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Rafiki suala la kujifunza ni endelevu halina ukomo. Pale unapopata ukomo wa kujifunza maana yake unajiandaa na kushindwa. Mara baada ya kumaliza elimu ya darasani kamwe usikubali kufanya hitimisho la kusoma.

Masomo mengi ambayo tunahitaji kujifunza inatakiwa kuwa na sehemu ambapo mtaala umeandaliwa utakaokuongeza hatua kwa hatua mpaka uweze kufuzu katika masomo hayo. Tofauti na elimu rasmi ya darasani ambapo unakuwa na mtaala maalum.

Huku katika maisha ya kila siku hakuna mtaala maalum bali unajifunza kutegemeana na mahitaji ya ujuzi husika. Hapa chini nakushirikisha shule mbili ambazo unaweza kuhudhuria masomo na kujifunza mambo mengi.

Soma Makala Hii Inayohusiana : Namna ya Kutambua Dalili Za Kushindwa

Shule ya kwanza unayoweza kuhudhuria ni uzoefu ulionao. Angalia historia yako mambo ambayo umekuwa ukiyafanya yamekujengea uwezo ambao una makosa uliyoyafanya unayoyaweza kuyakwepa kwa kutoyarudia lakini pia mambo uliyofanikiwa ambayo yanaweza kukusaidia kujikita zaidi na kuendelea kuyaboresha kuyatumia ili kukupatia mafanikio zaidi.

Shule ya pili unayoweza kuhudhuria ni kujifunza kwa wale walioshindwa na kufanikiwa katika lile eneo ambalo unalifanyia kazi. Angalia katika wale walioshindwa mambo yaliyowapelekea kushindwa na uyaepuke wakati huo huo ungalie pia wale waliofanikiwa uzingatie yale yaliyowasababisha wafanikiwe ili yakusaidie pia.

Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Goodluck Moshi
Author
StadizaMafanikio

Related Posts:

  • Njia Bora Ya Kukabili Changamoto YoyoteHabari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki maisha tunayoishi yana changamoto za aina mbalimbali. Changamoto hizi ni njia pekee ambayo kama utaiitumia vizuri itakusaidia … Read More
  • Uchambuzi Kitabu cha " MEGALIVING, 30 DAYS TO PERFECT LIFE"Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Robin Sharma ni mwandishi wa kitabu cha MEGALIVING, 30 DAYS TO PERFECT LIFE. Katika kibao hiki Robin anaeleza namna ambavyo unaweza k… Read More
  • Uchambuzi Kitabu cha " THE COMPOUND EFFECT"Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Darren Hardy ni mwandishi wa kitabu cha THE COMPOUND EFFECT. Katika kitabu hiki mwandishi anatueleza siri kubwa iliyopo katika kufany… Read More
  • Kwa Nini Unahitaji Kujifunza Jambo Jipya Kila Siku?Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki mabadiliko na ukuaji ni vitu viwili muhimu vyenye mchango mkubwa katika maisha tunayoishi kila siku. Maisha yanakua na ladha a… Read More
  • Namna Ya Kudelete File Katika KompyutaHabari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki moja ya operation ambayo inafanyika mara kwa mara katika matumizi ya kompyuta ni delete. Delete hufanya kazi ya kufuta file li… Read More

0 comments:

Post a Comment