Sunday, 27 November 2016

Namna Ya Kudelete File Katika Kompyuta

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Rafiki moja ya operation ambayo inafanyika mara kwa mara katika matumizi ya kompyuta ni delete. Delete hufanya kazi ya kufuta file lililopo katika sehemu au location katika kompyuta.

Kuna namna mbili ambazo unazoweza kutumia kufuta file katika kompyuta:

(a) Katika namna hii ya kwanza unachagua file unalotaka kulifuta kisha unabofya kitufe katika keyboard kilichoandikwa delete au unabofya kitufe cha kulia cha mouse na kuchagua delete.

Soma Makala Hii Inayohusiana : Jinsi ya Kutengeneza Bootable USB Drive

Mara baada ya kubofya, file litondolewa kutoka sehemu iliyopo kwenda katika recycle bin. Unaweza kulirudisha file ikiwa umelifuta kwa makosa kwa kubofya na kuchagua restore. Ikiwa pia unataka ulifute katika recycle bin basi rudia hatua za kawaida za kufuta file kama nilivyoelekeza hapo juu.

(b) Katika namna hii ya pili unachagua file unalotaka kulifuta kisha unabofya kwa pamoja (simultaneously) vitufe katika keyboard shift na delete.

Mara baada ya kubofya, file litaondolewa kutoka sehemu iliyokuwa lakini halitapelekwa katika recycle bin. Hapa unakuwa hauwezi kulirudisha file lilipokuwa. Hii hufahamika kama kudelete permanently

Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Goodluck Moshi
Author
StadizaMafanikio

Related Posts:

  • Swali la WikiNi kitu gani ungethubutu kukifanya ikiwa kama umehakikishiwa mafanikio kupitia kukifanya hicho kitu? What would you dare to try to do if you were guaranteed to succeed?… Read More
  • Salamu ya Mwezi AprilJambo la kwanza Simamia mawazo na shughuli zako kwa ufanisi wa hali ya juu Jambo la pili Kila unachokifanya kifanye kiwe na muonekano tofauti na ambavyo wengine wamezoea kukifanya kwa kuhakikisha kinaleta manufaa kwako pamoj… Read More
  • Mambo ya Kuzingatia UnaposhirikianaUnapoamua kushirikiana na mtu mwingine ni vizuri muweke msingi katika masuala 3 yafuatayo ili kuepuka kukatishwa tamaa kwa kutokuwa na ulinganifu wa matarajio na matokeo Jambo la kwanza: Fahamu kila mshirika nini atamiliki (… Read More
  • Usifanye Kosa Hili Katika BiasharaUnapoamua kuchagua kuwa utashirikiana na mtu mwingine kufanya biashara ya ndoto yako, usitumie kigezo cha huyo mshirika kuwa ni mmoja wa wanafamilia wako au ni mmoja wa marafiki zako wa karibu sana, utakuwa umejiingiza katika… Read More
  • Fanya Haya ili Ukue1. Usitamani mambo yangekuwa marahisi, tamani ungekuwa bora mno Don't wish it were easier; wish you were better 2. Usitamani ungekutana au ungekuwa na matatizo machache,tamani ungekuwa na ujuzi zaidi Don't wish for less prob… Read More

0 comments:

Post a Comment