Wednesday, 23 November 2016

Kwa Nini Unahitaji Kujifunza Jambo Jipya Kila Siku?

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Rafiki mabadiliko na ukuaji ni vitu viwili muhimu vyenye mchango mkubwa katika maisha tunayoishi kila siku. Maisha yanakua na ladha ambayo inatufanya kuendelea kuyafurahia kwa sababu ya mabadiliko na kukua.

Kujifunza ni jambo la muhimu zaidi ambalo tunahitaji kulipokea au kulikubali au kulifurahia kila wakati tunapopata fursa. Unaweza kujifunza mambo mengi mbalimbali kutegemeana na mapenzi na shauku ya maeneo ambayo unapenda kuwa na maarifa.

Soma Makala Hii Inayohusiana : Hii Ndiyo Njia Pekee ya Kutatua Matatizo Yako Yote

Unaweza kujifunza kutoka katika uzoefu alionao mtu au uzoefu ulionao, kutoka kwa mtu unayemfahamu, kutoka katika kitabu, kutoka katika semina,mkutano, kutoka kwa wazazi, kutoka kwa mtoto wako, mwenzi wako na kadhalika.

Kwa kadiri tunavyozidi kujifunza vile vile ndivyo tunavyozidi kukua na kuyapatia maisha yetu thamani zaidi. Rafiki unapojifunza usiende ukiwa na yale mambo unayoyafahamu tu na kuyang'ang'ania kuwa ndiyo sahihi na hutaki kupokea mambo mapya tofauti na unayofahamu , hapana rafiki unahitaji kuwa open ili uweze kuimarisha maarifa uliyonayo.

Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Goodluck Moshi
Author
StadizaMafanikio

Read, Apply and Share!

Related Posts:

  • Fahamu Haya Kama KiongoziKwa kila unayemuongoza unahusiana naye kwa kulingana na mojawapo kati ya ngazi hizi tano. Ngazi ya chini kabisa ni ngazi ya kwanza na ngazi ya juu kabisa ni ngazi ya tano: 1. Ngazi ya kwanza ambayo tunaanza nayo katika safar… Read More
  • Kanuni Inayoamua Wewe Kufanikiwa au KushindwaKatika mambo tunayofanya kuna matokeo mawili; aidha kufanikiwa sawasawa na malengo tuliyojiwekea kabla hatujanza kutekeleza jambo au kutokufanikiwa ambapo tunaweza kukuita kushindwa kutokana na kutofikia vigezo tulivyoviweka … Read More
  • Mbinu za Kustahimili MatatizoSiri moja kubwa ambayo imewafanya watu waliofanikiwa kuendelea vizuri ni mtazamo juu ya matatizo wanayokutana nayo. Ukizielewa kanuni hizi 6 kuhusu matatizo na kuzifanyia kazi ipasavyo wewe pia utakuwa mshindi. 1. Kila mtu a… Read More
  • Sumu ya MafanikioUnapokosa lengo kubwa katika maisha yako kwa kutokujua nini hasa unahitaji na unakipataje, mara nyingi hupelekea kutegemea maoni au ushauri wa watu wengine zaidi katika kuamua kitu cha kufanya kwa ajili ya maisha yako badala … Read More
  • Je, Umepoteza Ujasiri (Confidence)?Katika jambo lolote unalofanya unahitaji kuwa na ujasiri ili uweze kuwa na nguvu au stamina ya kuweza kulileta katika uhasilia(kulikamilisha) bila kujali vikwazo utakavyokutana navyo njiani. Zifuatazo ni njia au namna ambavy… Read More

0 comments:

Post a Comment