Inawezekana umefika katika hatua ambayo unaona kama
ungekuwa na kiasi fulani cha fedha basi matatizo yako yote ambayo
yamekuwa yanakusumbua au yanakukabili bila kujali yana umri kiasi gani
yangekuwa yamepatiwa ufumbuzi wa kudumu.
Kama
ingekuwa kuwa na fedha ni kupata ufumbuzi wa matatizo tuliyonayo ina
maana tungetarajia watu wenye fedha nyingi wangekuwa hawana matatizo
kabisa. Lakini katika maisha ya leo baadhi ya hawa watu ambao wana fedha
sana ndiyo ambao wana matatizo zaidi kama ya magonjwa, kukosa furaha
n.k ukiwalinganisha na wale ambao hawana fedha au wana fedha kiasi
kidogo.
Kwa mfano fedha haiwezi kukulinda usiumwe lakini inaweza
kukusaidia kupata huduma bora zaidi ya kiafya baada ya kuumwa. Kwa hiyo
tungekosea sana kusema kwa kuwa una hela basi umeshapona mara baada ya
kugundua unaumwa, bali unapokuwa unaumwa hatua ya kwanza ni kuanza
kufikiri namna ya kukupatia huduma ya afya inayoweza kutibu ugonjwa
unaokusumbua halafu hatua ya pili inafuata namna ya kutumia kiasi cha
fedha uliyonayo kupata huduma husika kutatua tatizo linalokukabili. Kwa
hiyo fedha huja katika hatua ya mbele sana na siyo hatua ya kwanza
katika utatuzi wa tatizo bali ni kitu kinachowezesha utatuzi wa tatizo.
Kwa mfano fedha haiwezi kukulinda usiumwe lakini inaweza
kukusaidia kupata huduma bora zaidi ya kiafya baada ya kuumwa. Kwa hiyo
tungekosea sana kusema kwa kuwa una hela basi umeshapona mara baada ya
kugundua unaumwa, bali unapokuwa unaumwa hatua ya kwanza ni kuanza
kufikiri namna ya kukupatia huduma ya afya inayoweza kutibu ugonjwa
unaokusumbua halafu hatua ya pili inafuata namna ya kutumia kiasi cha
fedha uliyonayo kupata huduma husika kutatua tatizo linalokukabili. Kwa
hiyo fedha huja katika hatua ya mbele sana na siyo hatua ya kwanza
katika utatuzi wa tatizo bali ni kitu kinachowezesha utatuzi wa tatizo.
Kwa maana nyingine fedha haina ubaguzi kwamba wewe ni
wa rangi gani au umetoka katika kundi gani la uchumi (mtu masikini au
mtu wa daraja la kati au mtu tajiri) au wazazi wako walikuwa na hali
gani ya kifedha au hata unafikiri kuwa wewe ni nani (nafasi yako katika
jamii).
Fedha haiwezi kubagua kwa kuwa
haijui mambo mengi yanayomhusu yule anayemiliki kiasi husika cha fedha.
Fedha haijui una kiwango gani cha elimu au maarifa, fedha haina masikio
wala macho wala uwezo wa kuhisi. Bali fedha ipo kwa ajili ya kutumiwa,
kuwekwa akiba, kuwekezwa.
Kila mmoja wetu
anayo haki na fursa sawa kuweka jitihada ya kupata fedha zaidi bila
kujali jana yako ilikuwaje. Inawezekana ukaona ni ngumu na kuna
changamoto na vikwazo zaidi lakini inawezekana kufanya na kuibadili
maisha yako.
Kwa hiyo ni muhimu sana kukaa chini na kutafakari na
kufafanua kwa kina ni nini hasa kusudi la wewe kuwa na kiasi cha fedha
unachokihitaji. Kuwa na ufafanuzi au maana sahihi ya wewe kuwa na kiasi
cha fedha unachokihitaji itakusaidia kuendana vema na tabia hizo kuu
tatu za fedha nilizoziainisha hapo juu (kutumiwa, kuwekwa akiba na
kuwekezwa).
Kitu Hiki Kimoja Ni Muhimu Kuliko Kiwango Cha Fedha Unachotaka.
Related Posts:
Mbinu za Kustahimili MatatizoSiri moja kubwa ambayo imewafanya watu waliofanikiwa kuendelea vizuri ni mtazamo juu ya matatizo wanayokutana nayo. Ukizielewa kanuni hizi 6 kuhusu matatizo na kuzifanyia kazi ipasavyo wewe pia utakuwa mshindi. 1. Kila mtu a… Read More
Sumu ya MafanikioUnapokosa lengo kubwa katika maisha yako kwa kutokujua nini hasa unahitaji na unakipataje, mara nyingi hupelekea kutegemea maoni au ushauri wa watu wengine zaidi katika kuamua kitu cha kufanya kwa ajili ya maisha yako badala … Read More
Je, Umepoteza Ujasiri (Confidence)?Katika jambo lolote unalofanya unahitaji kuwa na ujasiri ili uweze kuwa na nguvu au stamina ya kuweza kulileta katika uhasilia(kulikamilisha) bila kujali vikwazo utakavyokutana navyo njiani. Zifuatazo ni njia au namna ambavy… Read More
Fahamu Haya Kama KiongoziKwa kila unayemuongoza unahusiana naye kwa kulingana na mojawapo kati ya ngazi hizi tano. Ngazi ya chini kabisa ni ngazi ya kwanza na ngazi ya juu kabisa ni ngazi ya tano: 1. Ngazi ya kwanza ambayo tunaanza nayo katika safar… Read More
Kanuni Inayoamua Wewe Kufanikiwa au KushindwaKatika mambo tunayofanya kuna matokeo mawili; aidha kufanikiwa sawasawa na malengo tuliyojiwekea kabla hatujanza kutekeleza jambo au kutokufanikiwa ambapo tunaweza kukuita kushindwa kutokana na kutofikia vigezo tulivyoviweka … Read More
0 comments:
Post a Comment