Thursday, 2 July 2015

Jinsi ya Kujua Kama Unachofanya Ni Sahihi Katika Maisha Yako

Kila mtu anapokuja hapa ulimwenguni anakuwa amebeba maagizo maalum ambayo anatakiwa ayatekeleze kwa ajili ya kufanya ulimwengu kuwa sehemu bora ya kuishi. Njia nzuri ya kuweza kujua kile unachofanya kama ni sahihi ni kwa kuyafahamu maagizo uliyobeba ambayo hakuna mwingine zaidi yakeo anaweza kuatekeleza. Na maagizo hayo unaweza kuyafahamu kwa kuanza kujitathimini kwa njia ya maswali kama je umeshatambua maagizo uliyoyabeba? Au je una kipaji, uwezo, shauku gani ambayo ni ya kipekee kwako na hakuna mtu mwingine wa aina yoyote anayo isipokuwa wewe tu? Au ya mwisho ambayo ni nzuri zaidi ni kwa kuangalia kile unachokifanya na kujiuliza je unachokifanya ndicho ulichokusudiwa au sababu ya wewe kuwepo hapa ulimwenguni?
Hapa ninakuletea viashiria ambavyo vitakusaidia kujitathmini kama kwanza upo katika kada au eneo sahihi lakini la muhimu zaidi ni lile unalofanya katika hilo eneo ndilo lile unalopaswa au sababu yaw ewe kuwepo hapa ulimwenguni.
  1. Unakuwa unapenda kile unachokifanya kwa kuwa kinakuvutia , kinakupa shauku na mvuto wa kipekee kukifanya
  2. Unakuwa unataka kuwa bora sana katika kile unachokifanya. Na miongoni mwa asilimia kumi ya watu walio bora katika eneo au kada yako unataka na wewe uwepo
  3. Unawapenda wale wote ambao wako katika eneo au kada uliyopo na pia unapenda kufikia mafanikio ambayo wao pia wameyafikia
  4. Unapenda kujifunza kuhusiana na hilo eneo au kada yako kwa kusoma mambo yanayohusu kada yako, kuhudhuria semina au mihadhara ambayo inazungumzia mambo yanayohusu eneo au kada yako, kusikiliza program za sauti zilizorekodiwa kuhusiana na kada yako. Na zaidi hata iweje unakuwa huchoki kujifunza katika hilo eneo lako.
  5. Kada au eneo sahihi kwako ni lile ambalo kwako ni rahisi kujifunza na pia ni rahisi kuweka katika matendo yale uliyojifunza. Ila kwa wengine inaonekana ni vigumu na kwako inakuwa kawaida sana kufanya.
  6. Kutokana na kufurahia kile unachofanya unakuta muda unakuwa kama umesimama kwako na inaweza ikawa imekukolea sana hadi unasahau kula, kunywa hata kwend mapumziko
  7. Mafanikio unayoyapata katika eneo ndiyo inayokupa hamasa ya kipeekee na furaha adimu. Na pia unakuwa huwezi kuacha kusubiri au kukaa muda mrefu bila kufanya kitu kikusogeze hatua moja mbele upate mafanikio mengine
  8. Unapenda kufikiri kuhusu hilo eneo au kada yako na pia wakati haufanyi kitu unapenda kuzungumza kuhusu eneo au kada yako. Masiha yako yote yanakuwa yamezngukwa na mambo yanayohusu eneo au kada yako
  9. Unapenda kuwa na mahusiano na kuwa karibu na watu zaidi ambao wapo katika eneo lako.
  10. Na mwisho ni kuwa unapenda kufanya hayo unayofanya kwa maisha yako yote, hutaki kustaafu kuyafanya kwa kuwa unafarahia jinsi unavyoyafanya

Kwa kuweza kutambua eneo au kada yako sahihi ambayo unatakiwa uwe itakusaidia kupata mafanikio nah ii itakusaidia kuwelekeza moyo wako kufanya vizuri na vizuri zaidi. 

Related Posts:

  • Jinsi Ya Kuishinda Hofu Uliyonayo Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki katika maisha watu wamekuwa wakitawaliwa na hofu, wameipa hofu nafasi kubwa ya kutawala maisha yao. Hofu huzaa malalamiko ku… Read More
  • Mambo Matano (05) Yanayosababisha KushindwaHabari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki si wote wanajifunza kutokana na makosa wanayoyafanya au kutambua mapema makosa waliyoyafanya ili wasiyarudie. Kuwa na mwongozo… Read More
  • Mambo Matano (05) Yaliyojificha Katika Mafanikio Yako Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki watu wengi wamekuwa wakipima mafanikio kwa kiwango cha vitu vinavyomilikiwa na mhusika. Kutokana na hili kunakuwa na maana m… Read More
  • Namna ya Kutambua Dalili Za Kushindwa Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki gari linapopelekwa kwa fundi kwa ajili ya kutatua tatizo lililo nalo, litaweza kutatuliwa ikiwa tuu kisababishi cha tatizo h… Read More
  • Faida Tatu (03) za Biashara Inayoendeshwa Kwa Intaneti Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki katika zama za viwanda (industrial age) bidhaa nyingi zilizokuwa zinauzwa zipo physical kiasili. Bidhaa hizi mpaka uzinunue … Read More

0 comments:

Post a Comment