Wednesday 21 December 2016

Sababu Kumi (10) Zinazokuzuia Kuanza Biashara

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala mbalimbali zinazowekwa katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio.

Napenda kukupongeza kwa hatua uliyochukua ya kuamua kutembelea mtandao huu kwa ajili ya kuchota maarifa ambayo yatakusaidia katika maisha yako na pia kukushukuru kwa ajili ya kuwashirikisha marafiki wengine waungane nasi kwa ajili ya kuendelea kuboresha maisha yetu.

Katika makala yetu ya leo napenda kukushirikisha sababu kumi (10) ambazo zinatumika kama pazia la kujifichia au kisingizio cha kusababisha watu wasianze kutengeneza biashara zitakazohudumia watu na hatimaye kuwaingizia kipato.

1. Kukosa fedha (mtaji) kwa ajili ya kuanza biashara.

2. Kuwa na idadi kubwa ya ndugu au jamaa wanaokutegemea kwa ajili ya kuwasaidia kwa huduma mbalimbali kama mahitaji muhimu, elimu na kadhalika.

3. Kukosa mawasiliano na watu ambao wataweza kukuunga mkono katika biashara yako.

4. Kukosa uwezo wa kutosheleza wa kuanza , kuendesha na kusimamia biashara yako.

5. Kukosa muda wa kuendesha na kusimamia biashara kutokana na kutingwa na shughuli nyingine.

Soma Makala Hii Inayohusiana : Mambo Matano (05) Yanayosababisha Kushindwa

6. Kukosa mtu sahihi ambaye anaweza kukuongoza hatua kwa hatua katika biashara mpaka uweze kusimama mwenyewe.

7. Umri wako umeshakwenda sana.

8. Uhitaji wa muda mwingi kutoka kuanza biashara mpaka kukua na kuendelea.

9. Kuchukia kushughulika na wafanyakazi ambao unatakiwa kuwasimamia.

10. Hofu ya kuwa na biashara ni hatari (risky).

Rafiki hizi ni baadhi tu ya sababu zinazotumiwa, je ni sababu ipi umeitumia kujitetea kama hoja ya msingi ambayo inakuzuia mpaka sasa kuanza kutengeneza biashara?

Tafadhali nishirikishe maoni yako kwa kutaja sababu ipi ambayo unaona ndiyo kikwazo kikubwa au kunitajia sababu nyingine unazozifahamu, ili tuweze kuzijadili katika makala zijazo.

Rafiki napenda kukuarifu kuwa ikiwa una maswali au mada ambayo ungependa niiandikie makala , unaweza tuma katika anuani yangu luckmoshi@gmail.com

Goodluck Moshi
Mwandishi
StadizaMafanikio

Monday 5 December 2016

Jinsi ya Kuinstall Kapersky KIS 2017 Katika Microsoft Windows 7

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Ili kulinda programu na data zilizopo katika kompyuta muhimu kuweka programu ambazo zitazuia programu hatarishi kuathiri ufanyaji kazi wa kompyuta. Programu hatarishi hufahamika kwa jina la virusi (virus).
Na programu ambayo inazuia kompyuta kuathiriwa na virusi huitwa antivirus.

Kuna watengenezaji wengi ambao wanaandaa na kuuza hizi programu za antivirus. Baadhi ya antivirus ni Kapersky, McAfee, Avira, Escan, AVG na kadhalika.

Soma Makala Hii Inayohusiana Jinsi ya Kutatua Tatizo la Barua Pepe Kutoingia Katika Inbox

Katika makala hii napenda kukushirikisha namna ya kutatua changamoto ambayo unaweza kukutana nayo wakati unainstall Kapersky Internet Security 2017 (KIS 2017).

Changamoto moja kubwa ambayo nimekutana nayo wakati nafanya installation ya KIS 2017 katika Operating System ya Windows 7 Professional ni kuwa programu hizi mbili kutokuendana (compatible).

KIS 2017 inahitaji Windows 7 Professional Service Pack 1 ili ikubali kuwa installed. Ikiwa una Windows 7 Professional isiyo Service Pack 1 unahitaji kupakua (download) Service Pack 1 kwa kusearch katika Google na kisha kufanya installation.

Baada ya kufanya installation ya Service Pack 1 kwa mafanikio ndipo uendelee na kuinstall KIS 2017.

Tatizo hili la kuhitaji Service Pack 1 utalipata ikiwa Windows 7 ndiyo inatumika. Lakini hautakutana na tatizo hili ikiwa unatumia Windows 8 au Windows 10.

Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Goodluck Moshi
Author
StadizaMafanikio