Thursday 30 April 2015

Jambo Moja la Kuzingatia Ili Uwe Tajiri

Kabla ya kitu chochote hakijaweza kuwa katika hali yake ya uhalisia huanza katika wazo. Nyumba haiwezi kujengwa kabla ya kuanza kuwa na mchoro unaongoza ujenzi wa hiyo nyumba. Katika maana nyingine rahisi unaweza kusema tunafikiri kwanza alafu tunafuata utekelezaji au kuweka katika matendo kile tunachokifikiri.
Jaribio rahisi ambalo linaweza kukufanya ujue kama mtu ataishia kuwa tajiri au tayari ni tajiri ni kwa kutazama yale mambo anayoyafanya kwa kuwa yale anayoyafanya yanaweza kutabiri matokeo yanayotarajiwa.Mambo anayoyafanya mtu huyafnaya kutokana na mwongozo anaopata kutoka katika kiwanda chake cha kuzalisha mawazo.

Jaribio lenyewe ni kutazama mawazo ambayo anayatengeneza kupitia jinsi anavyoilisha akili yake. Chunguza ni mambo gani au vitabu vya aina gani au majarida ya aina gani au makala za aina gani huyo mtu anasoma. Katika hivo vitabu au majarida mwangalie vipengele gani ambavyo anavyovisoma na pia uangalie vipengele gani katika majarida au vitabu hivyo hivyo huwa havipi mkazo kuvisoma. Katika vile vipengele anavyovisoma chunguza anavisoma katika mpangilio gani au mfuatano upi?

Jaribio hili unaweza kulifanya hata kwako binafsi kama kweli una kiu ya kubadili hali yako ya sasa kuwa tajiri au kama tayari ni tajiri basi kuufanya utajiri wako ukue zaidi. Watu ambao ni matajiri walio kaa chini kutafakari na kuamua kwa kusudia kuwa wanataka kuwa matajiri tofauti na wale ambao labda wameshinda bahati nasibu au wamerithishwa mali huchagua vitabu au majarida ambayo yanaongeza thamani katika utajiri wao, huchagua vipengele katika majarida au vitabu ambavyo kweli vinaongeza thamani katika maisha yao, havipi mkazo vipengele vile ambavyo haviongezi thamani na katika haya majarida au vitabu utagundua huwa wanasoma viengele vinavyohusiana na fedha au biashara kwanza kabla ya kusoma vipengele vingine.

Ukitaka kuwa daktari ni muhimu sana usomee udaktari, au ukitaka kuwa msanifu majengo ni muhimu sana usome kuhusu masuala ya usanifu majengo ili uwe na uwezo wa kufanya kazi yako kwa ufanisi na usiwe mbabaishaji katika eneo husika ulilolichagua. Matajiri wote ambao wamechagua kwa makusudi kuwa matajiri wamejifunza kwa njia mbalimbali kuhusu utajiri. Mmoja wa wanamafanikio maarufu duniani Jim Rohn hupenda kusema ukihitaji furaha nenda ujifunze furaha, ukihitaji uhuru wa kifedha nenda ujifunze kuhusu uhuru wa kifedha, ukihitaji afya bora nenda ujifunze kuhusu afya bora, orodha hii inaweza kuendelea zaidi lakini Jim alihitimisha kwa kusema kila kitu unachokihitaji ni kujifunza, ndiyo maana nikasema kama unataka utajiri jifunze utajiri. Kujifunza huku sio kwa kukaa darasani kwa sababu mifumo yetu ya elimu haina mitaala inayowaelekeza watu namna ya kuwa matajiri bali ina mitaala ambayo inawaandaa watu kuwa waajiriwa. Matajiri wengi  waliamua kujiendeleza binafsi kwa kusoma makala, vitabu na majarida ambayo yanawapatia maarifa ambayo hayajawekwa katika mitaala ya mifumo wa elimu tulio nao.

Mafunzo makubwa ambayo wamejifunza ni namna ambavyo matajiri wengine kabla yao jinsi wanavyowaza kwa kudhibiti malighafi inayotumika katika kiwanda cha mawazo kupitia ulishaji wa akili zao kwa yale wanayoyasoma, wamejifunza namna matajiri waliotangulia wanavyofanya kazi, wanavyokula, wanavyoishi , wanavyoweka akiba, wanavyowekeza katika vitega uchumi mbalimbali.Wamejifunza kwa kujaribu kuongea na watu matajiri ili kuwapa mbinu za kufanikiwa kwa upande mmoja na kwa upande mwingine kuwaelekeza mambo ambayo wanatakiwa kuchukua tahadhari ili kuepuka kutetereka. Wamejifunza kwa kuuliza maswali sahihi, maswali sahihi ni yale maswali ambayo ukiuliza yanaenda kugusa na kubadili maeneo maisha yako moja kwa moja. Wamesoma mahojiano mbalimbali ambayo hawa matajiri waliotangulia wameyafanya, wamesoma kuhusu wasifu wa hawa matajiri waliotangulia. Hayo ndio masomo ambayo wanajifunza katika chuo cha utajiri.

Kama kweli umeamua kwa makusudi kabisa unahitaji kuwa tajiri ni lazima ujiendeleze kwa kuwa na uelewa pamoja na maarifa ya kujitosheleza kuhusu utajiri.

Zingatia Haya Ili Uifanye Siku Yako Bora

Mafanikio yako hayatokei siku moja, bali ni muunganiko wa siku nyingi ambazo umeishi kwa mafanikio.

Daima usiruhusu watu waiharibu siku yako kwa kuleta matatizo yao katika siku yako kwa njia yoyote mfano kwa kukuudhi. 

Unatakiwa uachane nao na uwe bize kufanya siku yako iwe bora zaidi

Thursday 23 April 2015

Kitu Hiki Kimoja Ni Muhimu Kuliko Kiwango Cha Fedha Unachotaka.

Inawezekana umefika katika hatua ambayo unaona kama ungekuwa na kiasi fulani cha fedha basi matatizo yako yote ambayo yamekuwa yanakusumbua au yanakukabili bila kujali yana umri kiasi gani yangekuwa yamepatiwa ufumbuzi wa kudumu.
Kama ingekuwa kuwa na fedha ni kupata ufumbuzi wa matatizo tuliyonayo ina maana tungetarajia watu wenye fedha nyingi wangekuwa hawana matatizo kabisa. Lakini katika maisha ya leo baadhi ya hawa watu ambao wana fedha sana ndiyo ambao wana matatizo zaidi kama ya magonjwa, kukosa furaha n.k ukiwalinganisha na wale ambao hawana fedha au wana fedha kiasi kidogo.

Kwa mfano fedha haiwezi kukulinda usiumwe lakini inaweza kukusaidia kupata huduma bora zaidi ya kiafya baada ya kuumwa. Kwa hiyo tungekosea sana kusema kwa kuwa una hela basi umeshapona mara baada ya kugundua unaumwa, bali unapokuwa unaumwa hatua ya kwanza ni kuanza kufikiri namna ya kukupatia huduma ya afya inayoweza kutibu ugonjwa unaokusumbua halafu hatua ya pili inafuata namna ya kutumia kiasi cha fedha uliyonayo kupata huduma husika kutatua tatizo linalokukabili. Kwa hiyo fedha huja katika hatua ya mbele sana na siyo hatua ya kwanza katika utatuzi wa tatizo bali ni kitu kinachowezesha utatuzi wa tatizo.

Kwa mfano fedha haiwezi kukulinda usiumwe lakini inaweza kukusaidia kupata huduma bora zaidi ya kiafya baada ya kuumwa. Kwa hiyo tungekosea sana kusema kwa kuwa una hela basi umeshapona mara baada ya kugundua unaumwa, bali unapokuwa unaumwa hatua ya kwanza ni kuanza kufikiri namna ya kukupatia huduma ya afya inayoweza kutibu ugonjwa unaokusumbua halafu hatua ya pili inafuata namna ya kutumia kiasi cha fedha uliyonayo kupata huduma husika kutatua tatizo linalokukabili. Kwa hiyo fedha huja katika hatua ya mbele sana na siyo hatua ya kwanza katika utatuzi wa tatizo bali ni kitu kinachowezesha utatuzi wa tatizo.

Kwa maana nyingine fedha haina ubaguzi kwamba wewe ni wa rangi gani au umetoka katika kundi gani la uchumi (mtu masikini au mtu wa daraja la kati au mtu tajiri) au wazazi wako walikuwa na hali gani ya kifedha au hata unafikiri kuwa wewe ni nani (nafasi yako katika jamii).

Fedha haiwezi kubagua kwa kuwa haijui mambo mengi yanayomhusu yule anayemiliki kiasi husika cha fedha. Fedha haijui una kiwango gani cha elimu au maarifa, fedha haina masikio wala macho wala uwezo wa kuhisi. Bali fedha ipo kwa ajili ya kutumiwa, kuwekwa akiba, kuwekezwa.

Kila mmoja wetu anayo haki na fursa sawa kuweka jitihada ya kupata fedha zaidi bila kujali jana yako ilikuwaje. Inawezekana ukaona ni ngumu na kuna changamoto na vikwazo zaidi lakini inawezekana kufanya na kuibadili maisha yako.

Kwa hiyo ni muhimu sana kukaa chini na kutafakari na kufafanua kwa kina ni nini hasa kusudi la wewe kuwa na kiasi cha fedha unachokihitaji. Kuwa na ufafanuzi au maana sahihi ya wewe kuwa na kiasi cha fedha unachokihitaji itakusaidia kuendana vema na tabia hizo kuu tatu za fedha nilizoziainisha hapo juu (kutumiwa, kuwekwa akiba na kuwekezwa).
  

Tuesday 14 April 2015

Sunday 12 April 2015

Salamu ya Mwezi April

Jambo la kwanza
Simamia mawazo na shughuli zako kwa ufanisi wa hali ya juu

Jambo la pili
Kila unachokifanya kifanye kiwe na muonekano tofauti na ambavyo wengine wamezoea kukifanya kwa kuhakikisha kinaleta manufaa kwako pamoja na jamii inayokuzunguka