Thursday, 2 July 2015

Aina Tano (05) za Uwekezaji Zinazoweza Kubadili Maisha Yako

Ili kuweza kuwa na utajiri endelevu katika maisha yako na unaojitosheleza ni muhimu ukawa mwekezaji. Uwekezaji upo wa aina nyingi. Hapa ninakuletea aina za uwekezaji unazoweza kuzifanya ili kukuwezesha wewe na wale watu wako wa karibu kuishi maisha ya utajiri wa kujitosheleza:




  1. Uwekezaji binafsi
Watu ambao wanatengeza utajiri wanafanya uwekezaji binafsi . hawa wanakuwa wasomaji kwa kujifunza. Daima huweka jitihada ya kujiboresha wao wenyewe siku hadi siku na kuongeza mipaka ya maeneo ambayo wanona wakijaribu watafanikiwa. Wanaongeza maarifa na uwezo wa kushawishi siku hadi siku. Na kiwango cha jitihada wanachoweka katika kujiboresha huwa kipo katika hali ya kukua siku hadi siku.

  1. Kuwekeza kwa wengine
Mwanamafanikio maarufu duniani Zig Ziglar alisema ukitaka kupata kitu chochote katika maisha ni vizuri uwasaidie wengine wapate vile wanavyovihitaji katika maisha yao. Watu wenye utajiri utagundua wamewekeza kuwasaidia wengine wafikie malengo yao na hivyo kusababisha na wao kufanikiwa kwa kuwafanikisha wenzao

  1. Wekeza katika taasisi
Katika taasisi unayofanya wekeza katika kuijenga taasisi hiyo ili iweze kuwa bora na taasisi inapoweza kuwa bora inawezesha kuongeza upataji wa mapato. Kuongezeka kwa mapato kwa taasisi kwa ujumla kunasaidia pia wale waliosababisha kuongezeka kwa mapato kuneemeka na hiyo faida. Kwa hivyo hili likifanyika katika kipindi chako cha kutumikia taasisi yako maanake utaongeza kujenga utajiri siku hadi siku.

  1. Wekeza katika mali zinazoongezeka thamani
Ubadilishaji wa fedha kwenda katika mali ambazo zinaongezeka thamani na zinafanya kazi badala yako siku hadi siku huongeza utajiri kwako. Mfano wa hili ni nyumba ambayo imejengwa kwa lengo la kupangasha au kukodisha. Sasa ile fedha uliyowekeza katika hiyo nyumba utaipata kwa kuendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka bila yaw ewe kufanya kazi.

  1. Wekeza katika mawazo

Vitu vingi tunavyoviona leo havikuanza moja kwa moja bila kupitia hatua Fulani, vingi vilianza kama wazo na kuendelezwa. Mawazo amabyo ni mazuri yakichanganywa na uchukuaji hatua wa kuyaweka katika matendo huleta matokeo mazuri ambayo yanaleta utajiri 

Related Posts:

  • Je, Umepoteza Ujasiri (Confidence)?Katika jambo lolote unalofanya unahitaji kuwa na ujasiri ili uweze kuwa na nguvu au stamina ya kuweza kulileta katika uhasilia(kulikamilisha) bila kujali vikwazo utakavyokutana navyo njiani. Zifuatazo ni njia au namna ambavy… Read More
  • Fahamu Haya Kama KiongoziKwa kila unayemuongoza unahusiana naye kwa kulingana na mojawapo kati ya ngazi hizi tano. Ngazi ya chini kabisa ni ngazi ya kwanza na ngazi ya juu kabisa ni ngazi ya tano: 1. Ngazi ya kwanza ambayo tunaanza nayo katika safar… Read More
  • Mbinu za Kustahimili MatatizoSiri moja kubwa ambayo imewafanya watu waliofanikiwa kuendelea vizuri ni mtazamo juu ya matatizo wanayokutana nayo. Ukizielewa kanuni hizi 6 kuhusu matatizo na kuzifanyia kazi ipasavyo wewe pia utakuwa mshindi. 1. Kila mtu a… Read More
  • Kanuni Inayoamua Wewe Kufanikiwa au KushindwaKatika mambo tunayofanya kuna matokeo mawili; aidha kufanikiwa sawasawa na malengo tuliyojiwekea kabla hatujanza kutekeleza jambo au kutokufanikiwa ambapo tunaweza kukuita kushindwa kutokana na kutofikia vigezo tulivyoviweka … Read More
  • Sumu ya MafanikioUnapokosa lengo kubwa katika maisha yako kwa kutokujua nini hasa unahitaji na unakipataje, mara nyingi hupelekea kutegemea maoni au ushauri wa watu wengine zaidi katika kuamua kitu cha kufanya kwa ajili ya maisha yako badala … Read More

1 comment: