Monday 24 October 2016

Uchambuzi wa Kitabu " TOUGH TIMES NEVER LAST BUT TOUGH PEOPLE DO"

Robert H Schuller ni mwandishi wa kitabu cha "TOUGH TIMES NEVER LAST BUT TOUGH PEOPLE DO" . Katika kitabu hiki mwandishi anatupa mbinu za kutumia tunapokuwa tunapitia vipindi vigumu katika maisha yetu ya kila siku. Hapa ninakushirikisha mbinu mia moja ambazo ukizitumia kipindi unapopitia magumu zitakusaidia kuvuka kipindi kigumu salama bila athari. Karibu tujifunze rafiki.



1. Watu wengi huwa wanapenda kushughulika na lawama badala ya kushughulika na tatizo
2. Tatizo huwa kubwa kama mtakosa mtazamo sahihi kuhusu tatizo husika
3. Ukiwa unatakiwa kuongea au kutoa tamko ili kushauri kitu na hauna cha kuongea , washirikishe historia yoyote inayokuhusu wewe
4. Hakuna mafanikio bila kutumia kanuni ya kuzidisha
5. Watu walio wakubwa kimafanikio ni watu wa kawaida ambao wana kiwango kikubwa cha maamuzi ambayo yamezidi maamuzi ya kawaida
6. Hakuna mtu anashindwa jumla kama atathubutu kujaribu kufanya    kitu cha thamani
7. Vipindi vigumu havidumu kamwe bali watu wagumu hudumu
8. Kitu ambacho tunatakiwa kukihofia ni hofu yenyewe
9. Kwa binadamu inaonekana haiwezekani lakini kwa Mungu mambo yote yanawezekana
10. Haiwezekani ukashindwa jumla kama utathubutu kujaribu
11. Ni muhimu kujifunza namna ya kutatua na kusimamia matatizo
12. Sio lazima kila tatizo liwe na ufumbuzi ingawa kila tatizo linaweza kusimamiwa vyema
13. Watu wanaofanikiwa ni wale ambao kamwe hawaachi kuamini
14. Ukifikiri kwa ukubwa na ukifanya kazi kwa juhudi, unaweza kufanya chochote unachotaka, unaweza kuwa vyovyote unavyotaka na unaweza kwenda popote unapotaka
15. Yaweke matatizo katika mtazamo sahihi usiruhusu tatizo likupatie udhuru
16. Mafanikio hayaondoi matatizo bali hutengeneza matatizo mapya
17. Mtu anayechagua kuyakwepa matatizo kiuhalisia anatengeneza matatizo mapya
18. Kila mwanadamu anayeishi anayo matatizo
19. Kila tatizo lina muda wake wa kuishi ambao ni ndogo
20. Matatizo huwa yanaisha
21. Hakuna tatizo litakalodumu kila tatizo litapita
22. Kila tatizo linabeba fursa ya kipekee
23. Kila tatizo litakubadilisha
24. Unao uwezo wa kuchagua tatizo likufanyie nini
25. Usipuuzie tatizo
26. Unao uwezo wa kukabiliana na tatizo
27. Mtazamo chanya hubadili tatizo lililokutoa machozi kukufanya uwe nyota kwa kukupatia uzoefu
28. Usilikuze tatizo kwa kuwa tatizo litapita
29. Hakuna mtu ambaye yuko kubadilishana matatizo na mwingine
30. Pambano kubwa ambalo wengi wanashindwa ni hofu ya kushindwa
31. Kadiri unavosubiri kutatua tatizo ndivyo unavopoteza wakati na fursa
32. Wewe binafsi ndio mwenye wajibu wa kutatua tatizo usimsubiri mtu mwingine
33. Hakuna mtu ambaye anashindwa mpaka anapoanza kulaumu wengine
34. Kila mwisho ni mwanzo mpya
35. Uongozi ni kitu ambacho kinachagua ndoto zako na kinaweka malengo yako
36. Maamuzi ya leo ndo uhakika wa kesho
37. Ni bora kujaribu kitu kikubwa na kushindwa kuliko kutokujaribu chochote na kuona umefanikiwa
38. Kushindwa hakuamaanishi wewe ndiye uliyeshindwa bali kunamaanisha hujafanikiwa bado
39. Kushindwa hakumaanishi hautimiza/haujafanikisha kitu bali kunamaanisha umejifunza kitu
40. Kushindwa hakumaanishi wewe ni mjinga bali kunamaanisha unayo imani ya kutosha
41. Kushindwa hakumaanishi umeabika bali kunamaanisha una nia ya kujaribu
42. Kushindwa hakumaanishi hauna mbinu za kufanya kitu bali kunamaanisha unahitaji kufanya kwa mbinu tofauti
43. Kushindwa hakumaanishi umepoteza maisha bali kunamaanisha unayo sababu ya kuanza tena
44. Kushindwa hakumaanishi ukate tamaa bali kunamaanisha kujaribu tena kwa jitihada zaidi
45. Kushindwa hakumaanishi hautakamilisha bali kunamaanisha jambo unalofanya litachikua muda mrefu
46. Kushindwa hakumaanishi Mungu amekuacha bali kunamaanisha Mungu ana mawazo mazuri zaidi kwa ajili yako
47. Hauhitaji kuhofia kushindwa unaweza kuwa mtu unayetaka kuwa
48. Usiruhusu tatizo likupe udhuru
49. Mtazamo ni muhimu zaidi kuliko ukweli
50. Kitu chochote cha kutisha kinapotokea usifanye chochote kwanza ila fikiri
51. Ni bora kufanya kitu kisicho kamili kuliko kutokufanya chochote kisicho na dosari
52. Tengeneza njia sehemu ambako hapatakuwa na njia
53. Usilitupilie mbali wazo kwa sababu haliwezekani lipe nafasi
54. Kamwe Usidharau thamani ya wazo
55. Unapoweza kubadili kisichowezekana kuwa kinachowezekana hayo ndio maendeleo (progress)
56. Hakuna Kushinda Kama hautaanza kufanya kitu
57. Hatua ya kwanza ya imani ni kujiamini wewe mwenyewe
58. Kama tatizo ulilonalo halijaisha je jiulize umelipatia kila ulichonacho kuhakikisha linaisha?
59. Ukiwa na imani Kama ya kuhamisha mlima hauwezi kushindwa ila ukiwa hauko tayari kulipa gharama ukashindwa
60. Hata ukiwa umezungukwa na kutokuwezekana kwingi inatakiwa usikate tamaa uendelee kuwa na imani
61. Unao uchaguzi wa kuendelea kuamini au kuacha katika kukifanikisha kile unachofanya
62. Unaweza kupumzika kwa kile unachokifanya kama unakutana na vikwazo vingi lakini sio kuacha moja kwa moja
63. Usikate tamaa hata kama mwendo unaonekana ni polepole
64. Pale mambo yanapokuwa mabaya zaidi ndipo hautakiwi kukata tamaa au kuacha kile unachofanya
65. Amini imani yako na kuwa na shaka na mashaka yako
66. Kufanya maamuzi ni rahisi kama hamna mkanganyiko katika mfumo wako wa uthaminishaji
67. Maombi ni nguvu muhimu inayovuta kila kitu ili kukufanikisha
68. Usikatishwe tamaa au kukosa ujasiri unapoambiwa hapana
69. Kuna rundo la kukataliwa kabla hujakubaliwa
70. Namna ya kutengeneza upya uimara (strength) wako
a) Tazama ulikopitia kipindi cha nyuma
b) Chunguza mambo yote yanayowezekana sasa
c) Andika gharama ambayo upo tayari kuilipa
d) Chagua jambo moja linalowezekana bila kujali gharama yake ni kubwa kiasi gani
e) Fanya kazi na uwe na subira
71. Tumaini na msaada huja katika muda ambao ameupanga Mungu
72. Mambo mema unayofanya leo yatasahaulika kesho ila we endelea kufanya mema
73. Ukifanikiwa utapata marafiki wa uongo na maadui wa kweli lakini we endelea kufanikiwa bila kujali
74. Tafuta furaha katika kufanya yale yaliyo mapenzi ya Mungu bila kujali yanatafsiriwa vipi au yanapokelewa vipi
75. Wakati watu wanapopitia magumu hutazama matatizo wanayopitia kuliko fursa zilizopo mbeleni wanakokwenda
76. Maisha ya leo ni mkusanyiko wa matokeo ya machaguo uliyoyafanya
77. Kufanikiwa katika maisha unahitaji mambo 2:
a) Kuanza kufanya kitu
b) Kuokuacha kukifanya hicho kitu ulichochagua
78. Kubali uhalisia kuwa utafanikiwa sehemu fulani kwa Namna yoyote tuu
79. Kwa maneno yoyote utakayochagua kiyatumia chagua maneno chanya na sio maneno hasi
80. Maneno hasi huleta matokeo hasi
81. Unastahili kufanikiwa Kama mtu mwingine yoyote anavyoweza kufanikiwa
82. Amini kwa namna yoyote mahali fulani kuna mtu atakusaidia kufanikiwa kufikia malengo yako
83. Amua kung'ang'ania kutimiza ndoto yako
84. Thubutu kujaribu kufanya kitu
85. Jipatie maarifa kila siku kwa kuwa na maarifa utakuwa na majibu sahihi kwa ajili ya watu wenye nguvu
86. Kuwa na mtazamo wa kutoa (giving) ndo siri ya mafanikio
87. Kadiri unavyopanda ndivyo utakavyovuna
88. Wanaofanikiwa ni wale wanaotoa jitihada/juhudi za ziada na wanaenda kupitiliza mipaka yao
89. Tumaini ni kuendelea kung'ang'ania , kuomba kwa matarajio ya kupata na kutokukata tamaa kamwe
90. Piga teke kukata tamaa au kukandamizwa
91. Yacheke matatizo yako
92. Kuwa tayari kuanza kidogo na kuongeza mipango kadiri unavyoendelea
93. Unahitaji kuwa na timu ya kufanya nayo mambo ili kufanikiwa
94. Acha kulalamika kwa sababu maisha hayawezi kuwa Kama unavyotaka
95. Funga mlango wa mambo yaliyopita yanakusononesha na utupe funguo wake usonge mbele
96. Kama bado hujafanikiwa unahitaji tu kujipanga tena upya
97. Kamwe usipoteze maono yako
98. Kabiliana na kila kilicho mbele yako ukiwa na Mungu Kama rafiki yako utafanikiwa
99. Elekeza maisha yako na matatizo yako kwa Mungu
100. Hakuna mbadala wa kufanikiwa bila kufanya kazi kwa juhudi
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako

0 comments:

Post a Comment