Utangulizi:
Kuna wakati mada ambayo unahitaji kuzungumza na hadhira hupelekea kuleta ugumu katika uwasilishaji kwa kujadiliana. Na hii hupelekea kuleta hata hofu kuona kama mahusiano yako na hadhira unayowasilisha majadiliano kuweza kubadilika. Changamoto hii huonekana hasa katika mada ambazo labda hazijazoeleka katika tamaduni za jamii husika au kuona zinagusa hisia moja kwa moja ya hadhira au kuona kama utaonekana ni mtu asiyejali. Majadiliano yenye ugumu namna hii huenda yakatokea katika mazungumzo yanayohusu binafsi, biashara , dini, siasa n.k.
Waandishi wa kitabu hiki wameweka mbinu ambazo zitasaidia kuweza kuwasilisha ujumbe hata kama unaonekana mgumu lakini pia kuendelea kulinda na kuyaboresha mahusiano ya pande zote mbili na kuacha pande zote zikiwa na furaha.
Mambo ya kujifunza na kuyafanyia kazi:
1. Kunapokuwa kuna mazungumzo ambayo yana ugumu ndani yake mara nyingi kunakuwa na mambo ambayo yanafikiriwa na mambo ambayo hayasemwi pia, na hofu ya kusema inatokea kutokana na kuona kuwa utaharibu mazungumzo zaidi, kunakuwa hakuna kuridhika na maamuzi yanayotokana na mazungumzo ya namna hii, maamuzi mengi yanayotokana na mazungumzo haya hufanywa kwa kuwa kiongozi tuu amesema
2. Kuna aina tatu za mazungumzo yenye ugumu:
a) Kitendo: mazungumzo ya namna huleta fikra ya kujiuliza ni nini kimetokea, jambo gani halikufanywa ipasavyo
b) Hisia: mazungumzo haya huhusisha namna mtu atakavyojisikia mfano kudharauliwa, kuumizwa na kadhalika
c) Utambulisho: mazungumzo haya huhusisha haiba ya mtu, yaani mtu amekuonaje kwa nafasi yako
3. Mara nyingi kunakuwa na kulaumu kwa nini upande wa pili umefanya vile umefanya katika shughuli mliyokubaliana na kupelekea kulaumu badala ya kutaka kuelewa kuwa kila mmoja ana mtazamo wake, matatizo yake na hivyo mnahitaji kuheshimu kila wazo la mmoja linapowekwa mezani na linatakiwa lipewe nafasi
4. Kunahitajika kuelewa (dhamira) dhumuni lililonyuma ya kile kilichotekelzwa na sio kuyatazama mambo kibinafsi na kuona kama umedharauliwa na kutoheshimika kwa mawazo au maelekezo yako umeyatoa
5. Ni vizuri pia kuheshimu hisia kutokana na yale yalikubalika kufanyiwa kazi, usifanye kitu kikamuumiza mtu na kuona amegandamizwa badala ya kuona amepewa nafasi ya kutenda ka uhuru na kufanya afurahie yale anayoyafanya
6. Kunapokuwa kuna mazungumzo ambayo ni magumu ni muhimu kuelewa mtazamo wa kila pande na kuona inaleta maana ipi katika lile suala mnalojadili ili kuweza kufikia muafaka , kwa hiyo ni muhimu kila mmoja apewe hiyo nafasi na sio kujibizana tuu maana hii ndo hatua muhimu ya kwanza kuelekea mabadiliko au kukubali mtazamo wa pande ya upinzani
7. Kila mtu anakuwa ana uchaguzi wa taarifa anazozingiza katika akili yake kutegemeana na mvuto alionao na hizo taarifa, kuna uwezekano wote mnaongea mada inayofanana ila kwa jinsi kila mmoja anavovutiwa na kipengele husika utakuta atatoa mchango wa mawazo kutegemeana na maslahi aliyonayo katika eneo hilo
8. Wakati mnapokuwa na mazungumzo magumu ni vizuri kama ukiwa unakataa mawazo ya mtu ukayakataa kwa uwazi, na pia lengo si kuonesha nani ameshinda bali ni kuonesha namna gani kila pande imeeeleweka na mawazo ya kila pande yamrjumuishwa pamoja
9. Kunapokuwa na mada unahitaji kuwasilisha kwa muhusika na ukiwa unafahamu kuwa wewe ndio upo sahihi na yeye hayuko sahihi, njia nzuri ni kwanza kuelewa namna anavyolielewa au kuamini kuhusu lile jambo na pia kufahamu wajibu wako wa kumsaidia ni nini katika hilo suala
10. Kosa kubwa linalofanyika katika mazungumzo huwa ni kufikiri tumepewa nia ya mtu bila kujua kuwa tunakuwa tunaelewa nia ya mtu kupitia hisia tulizonazo kutegemeana na kwamba tunaathirika kwa kiwango gani, inatakiwa hisia hizi ziwekwe pembeni
Hayo ni baadhi kati ya mengi niliyojifunza katika kitabu cha Difficult Conversation - How to Discuss what matters most
Mambo 10 yatakayokusaidia kuboresha Mawasiliano yako
Related Posts:
Maliza Robo ya Kwanza 2015 Hivi Hatua 3 muhimu unazohitaji kuzichukua ili kuweza kutumia muda wako kwa ufanisi na kupata matokeo ya ndoto yako kwa haraka: 1. Have a Plan Kuwa na mpango wa kina unaoanisha nini unachotaka kufanya na mpango huu ni lazima uw… Read More
Usipobadilika, utamezwa na mabadilikoYanapotokea mabadiliko jifunze kukabiliana nayo (kuadapt) kwa haraka vinginevyo utakavochelewa zaidi kwa kutafakari nini cha kufanya na kulialia na hali halisi utatumia gharama kubwa kuyapokea na muda utakuwa umekwenda pia. … Read More
Msingi wa kutimiza maisha yenye ufanisiUwezo uliopo ndani yetu ni mkubwa sana kuliko kile ambacho tumeshakitendea haki kwa nafasi zetu tulizonazo kwa kutendea ulimwengu. Maswali haya yatakusaidia kutafakari kitu gani ambacho unacho ndani yako bado hujakileta ulimw… Read More
Uwekaji Mipango UsioaminikaNi asili yetu kuwa na matumaini mema juu ya jambo fulani ambayo yamepitiliza uhalisia. Mfano tunadhani kuwa tutafanya mambo mengi kwa muda mchache kuliko inavyotakiwa kiuhalisia au kudhani jambo unalolifanya litachukua muda m… Read More
Fursa nyingi, Muda mchache na Rasilimali chache, Nifanyaje?Ukifanya uchambuzi kwa kulinganisha kundi la "shughuli na fursa" na kundi la "muda na rasimali" utapata hitimisho ya kuona katika kundi la "shughuli na fursa" zipo nyingi kuliko kundi la "muda na rasilimali" tulizonazo kwa aj… Read More
0 comments:
Post a Comment