Monday, 7 November 2016

Dondoo Tatu (03) Zitakazokusaidia Kupata Mada za Kuandika Katika Blogu

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!



Rafiki kati ya maswali yanayoulizwa na waandishi wanaanza kuandika (beginners) ni mada gani waichague kuandika makala katika blogu. Lakini pia kwa wale ambao wameanza kuandika huwa wanajiuliza nijikite katika mada gani katika kuendelea kuandika makala katika blogu.
Katika makala hii napenda kukushirikisha maeneo matatu ambayo tunakutana nayo au tumeshakutana nayo (common) lakini tumekuwa hatuyapi kipaumbele au kuwa na mtazamo wa kupata mada za kuandika katika blogu zetu.

Soma Makala Hii Inayohusiana; Hatua Nne (04) Katika Uandishi wa Blogu

(a) Andika kuhusu mada unayopenda kujifunza.
Kwa mfano ukikuta unapenda kusoma au kununua vitabu vya masuala ya mafanikio, basi fahamu hilo ni eneo mojawapo ambalo unaweza kuandika. Pia ikiwa una mtu ambaye ni mtaalamu wa kada fulani unayependa kumuuliza maswali kwa ajili ya kujifunza , basi fahamu hilo ni eneo lingine pia unaweza kuandika.
Rafiki ukiyaandika haya ambayo unajifunza unakuwa umewasaidia wengine kupata maarifa ambayo umejifunza.
(b) Andika kuhusu mambo unayopenda kufanya
Ukitafakari miaka yako mitano iliyopita, utagundua kuna kitu au vitu fulani umekuwa unapenda kuvifanya. Katika vitu hivi utagundua kuna mambo umekuwa ukiyafanya yakisukumwa na shauku ya wewe kuyafanya.
Rafiki unaweza ukayaona haya mambo ni ya kawaida kwako, lakini kuna watu ambao wanashauku na wanapenda kufanya mambo sawasawa na wewe ulivyoyafanya lakini hawana watu wa kuwasaidia kuwaongoza, ukiyaandika utakuwa umewasaidia kuwa role model wao kupitia yale unayoyaandika.
(c) Andika kuhusu mambo uliyopitia katika maisha yako
Kutokana na sehemu ulizoishi au sehemu ulizofanya kazi kuna uzoefu ambao  umekuwa ukiujenga hatua kwa hatua, siku hadi siku. Uzoefu huu ni hazina kubwa ambao unaweza kuwasaidia wale ambao wanaanza katika maeneo hayo.
Rafiki mambo haya uliyoyapitia katika maisha unaweza kuandika ili kuwasaidia waweze kuepuka makosa ambayo wewe uliyafanya  lakini pia waweze kutumia muda mfupi zaidi kuliko ambao uliuutumia kutokana na kukosa kocha wa kukusaidia.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Sunday, 6 November 2016

Uchambuzi wa Kitabu cha " SUCCESS SECRETS OF THREE TIME OLYMPIAN"

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!




Ruben Gonzalez ni mwandishi wa kitabu "SUCCESS SECRETS OF THREE TIME OLYMPIAN" . Katika kitabu hiki ameeleza mambo ambayo amekuwa akiyafuatilia na kujifunza kutoka kwa watu waliofanikiwa. Baada ya kujifunza alianzia  kuweka katika matendo yale ambayo alijifunza kutoka kwa watu waliofanikiwa, na hatimaye kanuni au mbinu zile zile zilimsaidia kufanikiwa pia. Hapa ni nakushirikisha mbinu au kanuni ambayo Ruben ameyaleeza.
1. Fanya maamuzi leo ya kuwa mwanamafanikio kwa kuwa tayari/nia ya kulipa gharama inayohitajika ili kuweza kufikia ndoto yako
2. Mafanikio hayapimwi na hatua uliyofikia leo bali hupimwa na vizuizi ambavyo umevivuka mpaka kufikia mafanikio
3. Watu waliofanikiwa hujiandaa na kujiweka katika nafasi sahihi kuweza kutumia fursa yoyote ambayo inaweza kujitokeza kuwasaidia katika safari ya mafanikio
4. Mtazamo wako juu ya jambo fulani unaamua kiwango chako cha kufanikiwa, kufikiri chanya kunakupa njia nyingi za kuweza kukusaidia kufanikiwa
5. Jipe nafasi ya kujifunza ujuzi, maarifa yanayoweza kukufikisha kupata ndoto zako
6. Iruhusu sheria ya wastani ifanye kazi katika maisha yako, kwa kadiri unavyoshindwa katika jambo fulani unapata mafunzo mengi ambayo yatakusaidia kufanikiwa kutokana na kujaribu njia nyingi za kufanikiwa
7. Unahitaji kujiamini wewe mwenyewe na kuamini kuwa utafikia ndoto yako.
8. Unapokuwa na mtazamo wa kuwa na utayari wa kufanya lolote linalokuhitaji bila kujali muda utakaoutumia ili kufikia mafanikio basi   kufanikiwa ni suala ambalo la kitambo kidogo
9. Vinaweza vikachakuliwa vitu vyote katika maisha yako ukabaki hauna kitu lakini kitu kimoja hubaki na wewe muda wote ni nguvu ya kuchagua, chagua leo namna unavyoitikia (react) katika hali yoyote inayokutokea
10. Daima weka malengo yako mbele yako
11. Fikiria mawazo ambayo yatakuhamasisha kufikia malengo kwa kuwa like unachokifikiria muda wote ndicho kitakachokutokea katika uhalisia
12. Kila kitu hutokea kwa sababu, changamoto tunazopata katika safari ya mafanikio ni kwa ajili ya kutupatia masomo makubwa ya kujifunza ili kuweza kuwa na uuanzaji sahihi katika jambo tunalofanya na pia kuweza kufikia mafanikio
13. Unahitaji kuwekeza nguvu zako katika lengo moja mpaka ufanikiwe ndio uelekeze nguvu zako katika lengo lingine mpaka malengo yako yote yaishe/yakamilike, usielekeze nguvu katika lengo zaidi ya moja kwa kuwa kiwango cha kufanikiwa kitapungua
14. Ujasiri hutokana na muda ambao umewekeza katika masaa, siku ili kujijengea maarifa na ujuzi wa kuwa bora katika fani unayoifanya
15. Changamoto kubwa kuliko zote kuelekea kufanikiwa ni kujitawala mwenyewe, utashawishika kufanya vitu ambavyo vitakuweka nje ya mstari wa Mafanikio, lakini siku zote katika Yale unayofanya jiulize swali moja kuwa je unachokifanya kinakusaidia kukusogeza Karibu na kufanikiwa
16. Jifunze masuala ya uongozi na uwasaidie wengine kwa kuwajenga kiujuzi ili waweze kuwa na ujasiri wa kuungana na timu yako ili kuweza kukusaidia kufikia mafanikio yako
17. Ujasiri katika kufanikiwa hutokana na utayari wa kuweka mambo katika matendo na kuvumilia.
18. Bila kujali shida unayoipata ni ya namna gani jifunze kuiongelesha na kuiambia kuwa wewe ni mkubwa mno kuliko hiyo shida na haitaweza kukushinda
19. Kila Mafanikio makubwa ni mjumuisho wa mafanikio madogo madogo
20. Jifunze kutokana na makosa yako, fanya marekebisho yanayohitajika alafu jiweke katika nafasi sahihi ya kutumia fursa inayokuja mbele yako
21. Shauku yako ya kufanikiwa itakupa nguvu ya kukusaidia usiachie njiani unachokihitaji na pia itakupa njia za kuweza kufanya ili ufanikiwe
22. Fanya zaidi ya kile kinachotarajiwa
23. Ukiamini kuwa unachokitaka kuwa kinawezekana na ukatenda mambo ambayo yanasaidia kukfanikisha unachotaka, ulimwengu nao utakusaidia kufanya ndoto, mipango na matarajio yako katika uhalisia
24. Tumaini hutuonyesha vile visivyoonekana na kutupatia vile visivyowezekana
25. Usiruhusu hofu ikutawale, hofu inatawaliwa kwa kutenda yale unayoyahofia
26. Usijudge siku kwa mavuno uliyoyapata bali judge kwa mbegu uliyootesha/uliyopanda
27. Ulimwengu daima humpatia mtu fursa ya kufanikiwa ikiwa maneno na matendo yake yanaonesha anajua anapoelekea
28. Kila siku kitu cha kwanza andika malengo yako
29. Amua kuwa mwanafunzi wa kudumu wa mafanikio
30. Vitabu unavyosoma na watu unaokutana nao vinaamua wapi utakuwa miaka mitano ijayo
31. Furaha ni zao la mambo matatu:
a) ubora wa mahusiano na watu wako muhimu
b) kiwango cha kudhibiti hisia zako
c) kutumia vipawa vyako kufikia malengo yako
32. Haijalishi unaanguka mara ngapi katika safari ya Mafanikio simama endelea na safari
33. Watu waliofanikiwa wanawekeza muda wao kutafuta njia za kufanikiwa zaidi
34. Fall in love with the process of making you succeed
35. Tafuta watu ambao wana ujuzi na rasilimali ambazo unahitaji ili kuweza kufikia mafanikio unayoyahitaji
36. Tafuta mshauri au kocha ambaye ataharakisha mafanikio yako
37. Leaders make decision all time. Followers make suggestions.
38. Kama unapitia mapambano katika maisha , unaandaliwa kwa ajili ya malengo makubwa na muhimu
39. Viongozi wapo tayari kufanya lolote linatakiwa kufanywa na wao ili kuboresha matokeo
40. Hauwezi kufanikiwa kupata kitu kikubwa katika maisha mpaka utakapoanza kuamini kuwa kuna kitu kikubwa ndani yako kuliko hali au mazingira unayoikabili
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Saturday, 5 November 2016

Uchambuzi wa Kitabu The Top Ten Distinctions Between Winners and Whiners

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!



Keith Cameron Smith ni mwandishi wa kitabu "THE TOP TEN DISTINCTIONS BETWEEN WINNERS AND WHINERS ". Keith anatushirikisha mbinu ambazo washindi wamekuwa wakizitumia kila mara wanapokuwa wanafanya kazi yoyote ili kuwasaidia kuwapa ushindi. Keith anasisitiza kuwa adui mkubwa anayechangia katika kushindwa ni tabia ya ulalamikaji, hali ya kukataa kuwajibika.
Keith anaamini kwa kusoma kitabu hiki ni njia mojawapo ya kuweza kukushirikisha mambo chanya yatakayochangia katika kukufanya uwe mshindi. Hivyo katika makala napenda kukushirikisha mambo ambayo nimeyapata kutoka katika kitabu hiki.
1. Kuwa mshindi sio tukio linalotokea katika muda mfupi, ni safari ndefu ya maisha
2. Maisha hayakwendi sawa sawa na mipango inasemekana maisha ni vile yanavyokwenda wakati unaendelea kupanga mipango
3. Uwajibikaji ni kufanya kile kilicho bora kwa nafasi yako au uwezo wako ukiwa na imani kuwa utapata matokeo mazuri
4. Ushindi ni mchezo unaohitaji timu na umoja
5. Hofu ni imani ya kuwa kitu kibaya kabisa kitatokea
6. Hofu imejengwa katika mizizi kuwa hauna machaguo
7. Ili uweze kuwa mshindi unahitaji kuwajibika kwa kufanya uchaguzi wa imani chanya zidi ya hofu
8. Washindi hujua kuwa daima wana machaguo na wanawajibika na hayo machaguo
9. Machaguo yanaamua hali, hali haiamui machaguo
10. Ni sahihi kusikitika kuhusu mategemeo fulani lakini si sahihi kukata tamaa
11. Ushindi huanza na mawazo na kuwaibika kufanya machaguo yale yaliyo chanya tuu
12. Washindi wana mtazamo wa mawazo yao ndio mbegu, na akili yao ndio udongo wa kukuzia mbegu, mawazo unayoyaweka katika akili yako huota mizizi na kisha kukua kuwa mti unaozaa matunda, kwa hiyo ni muhimu sana kuchagua ni mawazo ya aina gani unayoyaruhusu kukaa akili mwako
13. Washindi huamini wanawajibika na matokeo wanayoyapata
14.  Kwa kudhibiti mawazo yako unabadilisha matokeo yako, washindi huwajibika kwa matokeo yao kwa kudhibiti mawazo yao
15. Washindi wako tayari kulipia gharama inayohitajika ili waweze kushinda
16. Washindi hujifunza kutoka kwa wale walio bora zaidi yao kufanya vile wanavotakiwa kuvifanya ili kufikia hatua kama za hao walio mbele yao
17. Inawezekana ukajifunza na kupata kile unachotamani kukipata
18. Gharama kubwa washindi wanayolipa ni kupata maarifa
19. Mipaka uliyonayo katika kufanikiwa ni kwa sababu ya kukosa maarifa, waliofanikiwa zaidi yako ni kwa kuwa wana maarifa ambayo hauna na pia wameamua kuweka katika matendo yale maarifa waliyoyapata
20. Gharama nyingine inayolipwa na washindi ni upinzani, washindi hawajali watu wengine wanawafikiriaje bali wanajali wao wenyewe washindi wanajifikiriaje binafsi
21. Washindi hawawasikilizi wapinzani bali wanasikiliza mioyo/nia yao inavowaelekeza
22. Watu hawana muda na maisha yako hata kukufikiria, hata pale mtu anapokuwa mpinzani wako dakika tano baadae hata hana mawazo kuhusu wewe
23. Washindi wako tayari kulipa gharama ya kuwahudumia wengine kwa moyo mmoja kwa sababu kwa kuwahudumia wengine kupata kile wanachokihitaji kunakusaidia kuweza kupata chochote unachohitaji
24. Ongeza maarifa juu ya kile unachokitaka katika maisha yako, wapuuzie wapinzani na wahudumie watu kwa moyo mkunjufu
25. Malipo ya gharama hayatupatii tunachokitaka bali yanatupa fursa ya kukipata ( The payments don't give you what you want they only give you the opportunity to get it)
26. Usiruhusu mtu akuambie nini huwezi kufanya, ukihitaji kitu nenda ulipe gharama unayohitaji ukipate
27. Washindi huamini kuna njia ya kutupeleka katika mafanikio kwa kila jambo
28. Washindi hutazama matokeo wanayoyataka kwa umakini, wakiona hawajapati kama wanavotarajia wanarekebisha matendo yao (actions) hadi waweze kupata matokeo wanayoyahitaji
29. Washindi hulisha imani yao na kuifisha hofu
30. Kwa kawaida maono hutuonesha mwisho wa safari
31. Baadhi ya masomo utakayojifunza wakati was kuelekea mafanikio yako ni kushindwa, kukataliwa na kupoteza vitu.
32. Washindi hawalalamiki bali huthamini maisha. Huthamini kwa kuongea vitu vizuri vilivyotokea awali, vinavyotokea sasa na vitakavyotokea baadaye
33. Changamoto ya mabadiliko katika maisha
Nenda kwa siku kumi mfululizo bila kulalamika, ikiwa utalalamika kabla ya siku kumi hazijaisha bila kujali upo siku ya ngapi utakuwa umefuta zile siku zote ambazo ulifanikiwa kupita bila kulalamika kwa hivyo unatakiwa uanze mpya
34. Unahitaji kuwa msikivu zaidi kuliko unavyoongea, sikiliza kwa lengo la kuelewa unachoambiwa na si kwa lengo la haraka ya kujibu ulichokuwa unaambiwa
35. Kama unapitia wakati mgumu sasa kuna uwezekano mkubwa kuna baraka zilizojificha
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Friday, 4 November 2016

Mbinu Tano (05) Zitakazomzuia Mteja Wako Kukasirika

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Unaposhindwa kukidhi mahitaji ya mteja sawasawa na matarajio yake, au mteja anapoona mtoa huduma anamkwepa au mteja anapokosa ushirikiano kutoka kwa mtoa huduma , au anapokuwa hana furaha na huduma aliyopatiwa,hii hali humfanya mteja apate hasira.




Kama utakosa umakini namna ya kumhudumia mteja wa namna ambaye kimsingi tayari amejeruhiwa ,itakusababisha kumpoteza mteja huyo moja kwa moja. Hivyo ni muhimu kwa kila mmliki wa biashara au mtoa huduma yoyote kuhakikisha kuna mikakati thabiti iliyowekwa ambayo inaelekeza namna ya kuhudumia mteja mwenye hasira au mteja ambaye hana furaha.
Katika makala ya leo rafiki napenda kukushirikisha mbinu ambazo unaweza kuitumia kama mwongozo pia kukusaidia unapokutana na aina hii ya wateja.
(a) Epuka kuahidi kwa mteja kumpatia huduma au bidhaa ambayo hauna uhakika na uwezo wa kumpatia. Ahidi yale mambo ambayo unauhakika yapo ndani ya uwezo wako na unaweza kuyatimiza kwa kiwango kizuri.
(b) Fahamu kwa kina matarajio ambayo mteja anayo katika huduma au bidhaa anayotarajia kupokea kutoka kwako na uhakika wa uwezo wako kukidhi matarajio ambayo amekueleza.
(c) Ikiwa kuna mazingira yametokea na imesababisha ugumu wa kuweza kutimiza ahadi uliyoweka kwa mteja, kwanza ni vizuri uwe wazi na mkweli kwa mteja wako kumuelewesha kuwa hutaweza kutimiza ahadi, pili nenda hatua ya ziada umpatie mteja huduma au bidhaa mbadala ili kuokoa muda wake na pia kupunguza usumbufu.
(d) Ni muhimu na daima hakikisha mteja anapokea mrejesho kutoka kwako kuhusiana na mwenendo au hatua ulizofikia katika kuhakikisha unamridhisha. Kuwa na taarifa ni kuwa na nguvu (information is power).
(e) Jaribu kuwa na picha mapema jinsi ambavyo mteja atapokea kutoka kwako taarifa ambayo ipo kinyume na matarajio yake ili iweze kukusaidia kufanya maandalizi mazuri kabla hujakutana na mteja.
Rafiki mbinu hizi ni muhimu sana katika kukusaidia kuepuka kuingia katika kipindi kigumu cha kukuudhi mteja.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Thursday, 3 November 2016

Jinsi ya Kutatua Tatizo la Barua Pepe Kutoingia Katika Inbox

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Barua pepe ni njia ambayo watumiaji wa kompyuta hutumia kutuma ujumbe kwa njia ya kidigitali. Kuna kampuni za aina mbalimbali ambazo zinatoa huduma hii. Baadhi ya kampuni ni Google, Yahoo na kadhalika. Ili uweze kupokea na kutuma ujumbe kwa njia ya barua pepe ni lazima uwe na akaunti katika kampuni hizi. Akaunti hizi huwa hazihitaji malipo.

Makala Inayohusiana: Faida Nne (04) Unazopata Ukiwa na Akaunti ya Gmail.

Kawaida ujumbe unapoingia katika akaunti yako ya barua pepe unapaswa kukaa katika sehemu inayoitwa inbox. Kwa maana nyingine ujumbe ukiingia sehemu nyingine isipokuwa inbox inakuwa si kawaida. Katika makala hii napenda kukushirikisha hatua unazopaswa kufuata ikiwa utakuta barua pepe imeingia katika sehemu nyingine yoyote badala ya inbox.

(a) Ingia katika akaunti yako ya barua pepe ya Yahoo.

(b) Nenda upande wa kulia juu kuna sehemu ina alama kama ya gia,kisha bofya sehemu iliyoandikwa settings.



(c) Bofya sehemu iliyoandikwa Filters.Katika kiboksi kitakachotokea kunatakiwa kusiwe na kitu chochote.Ikiwa utakuta maandishi yoyote , yachague kwa kubofya maandishi yaliyopo , kisha katika sehemu ya juu bofya sehemu iliyoandikwa Remove



(d) Baada ya hatua (c) bofya kitufe cha Save kilichopo upande wa kushoto chini ili kukamilisha.

Hatua hizi ni kwa ajili ya akaunti za barua pepe za Yahoo tu.

Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako

Wednesday, 2 November 2016

Jinsi ya Kufanya Partition Katika Hard Drive

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Partition katika kompyuta ni kitendo cha kugawa hard drive katika sehemu mbalimbali. Kitendo hiki husaidia kutenganisha sehemu ya hard drive ambapo umeweka operating system kutokuchanganyika na sehemu ya hard drive ambayo utakuwa unaweka data zako. Hii inasaidia sana kuzuia data zako kuathiriwa (corrupted).

Makala Inayohusiana :Jinsi ya Kutengeneza Bootable USB Drive

Katika makala hii ninapenda kukushirikisha hatua kwa hatua jinsi unavyoweza kufanya partition ya hard drive katika kompyuta amabayo imekuwa installed Microsoft Windows 7.

(a) Baada ya kuwasha kompyuta yako nenda katika sehemu ya start iliyopo kushoto chini.





(b) Bofya kwa kutumia kitufe cha kulia cha mouse katika neno Computer, kisha tafuta neno Manage na bofya hapo.



(c) Bofya katika neno Disk Management ili uweze kuona hard drive zote ambazo zipo katika kompyuta yako. Angalia iliyoandikwa Disk 0 ndiyo ambayo utaitumia.



(d) Bofya kwa kutumia kitufe cha kulia cha mouse katika hard drive unayohitaji kufanya parrtition na kisha uchague maneno yaliyoandikwa Shrink Volume.



Makala InayohusianaJe, Unafahamu Kifaa Kinachoitwa Mouse?

(e) Baada ya hatua (d) bofya neno shrink ili kukamilisha.

(f) Baada ya hatua (e) utapata partition ambayo imeandikwa Unallocated na rangi yake itakuwa nyeusi kwa juu, bofya kwa kitufe cha kulia sehemu hiyo na uchague maneno create new simple volume na unapofika mwisho kabisa utatakiwa kuchagua neno Finish  ili kukamilisha hatua zote.




















Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako

Tuesday, 1 November 2016

Mfumo Pekee Utakakokusaidia Kukidhi Mahitaji ya Mteja

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Suala la kukidhi mahitaji ya mteja unaowahudumia linakwenda sambamba na utoaji wa huduma bora kwa mteja. Kiwango cha kukidhi mahitaji ya mteja hupimwa na jinsi unavyoweza kutimiza mahitaji ya mteja kuzidi ahadi uliyompa kabla hujampatia huduma.


Rafiki usipende kukisia au kuhisi matarajio ya mteja kupitia huduma unayotoa, unahitaji kujifunza kumuuliza mteja kuhusu matarajio yake. Jambo lingine ni kuwa matarajio ya mteja huwa yanabadilika mara kwa mara na yataendelea kuwa yanabadilika, hivyo unahitaji kutambua au kuyajua matarajio haya katika hali ya uendelevu (on-going basis).
Katika makala hii ninapenda kukushirikisha mambo machache ambayo yatakusaidia kuhakikisha unakidhi mahitaji na matarajio ya mteja kupitia huduma anyaopokea kutoka kwako.
(a) Tambua mahitaji ya mteja
Ikiwa kama hutambui mahitaji ya mteja wako ni vigumu sana kumridhisha au kukidhi matarajio yake anapopokea huduma yako. Kuna njia mbalimbali zinazoweza kukusaidia kutambua mahitaji ya mteja wako. Baadhi ya njia ni malalamiko kutoka kwa mteja , mrejesho kutokana na matumizi ya huduma yako, hoja mbalimbali (query) na tafiti.
(b) Jibu mahitaji ya mteja
Baada ya kutambua mahitaji ya mteja hatua inayofuata ni muhimu kuhakikisha unakidhi au unajibu mahitaji ya mteja. Kutegemeana na njia iliyotumika kutambua mahitaji ni muhimu kukawekwa mkakati sambamba ambao utajibu mahitaji husika. Ni muhimu pia kuwa na utaratibu ambao uko wazi unaoweza kupimika hata kwa wasaidizi wako , mfano ni muda ambao utachukua kutoka ulipopewa malalamiko na mteja mpaka muda ambapo umemjibu.
(c) Utunzaji wa kumbukumbu
Ni muhimu kuwa na mfumo ambao utahifadhi au utarekodi mahitaji ambayo yamepokewa kutoka kwa mteja, na majibu ambayo amepatiwa mteja. Hii itakusaidia kuwa na taarifa muhimu ambazo zinaweza zikatumika muda wowote. Pia itakusaidia katika tathmini ya jinsi unavyokidhi mahitaji ya mteja wako na uwekaji wa utaratibu mzuri utakaosaidia kuoanisha aina ya mahitaji kutoka kwa mteja na uwezo wa wasaidizi wako ambao wanaweza kujibu vizuri mahitaji hayo.
Kwa kuzingatia mambo hayo niliyoyaeleza hapo juu, huduma yako itaendelea kuwa hai au kudumu au kuwa endelevu (sustainable).
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako