Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Barua pepe ni njia ambayo watumiaji wa kompyuta hutumia kutuma ujumbe kwa njia ya kidigitali. Kuna kampuni za aina mbalimbali ambazo zinatoa huduma hii. Baadhi ya kampuni ni Google, Yahoo na kadhalika. Ili uweze kupokea na kutuma ujumbe kwa njia ya barua pepe ni lazima uwe na akaunti katika kampuni hizi. Akaunti hizi huwa hazihitaji malipo.
Makala Inayohusiana: Faida Nne (04) Unazopata Ukiwa na Akaunti ya Gmail.
Kawaida ujumbe unapoingia katika akaunti yako ya barua pepe unapaswa kukaa katika sehemu inayoitwa inbox. Kwa maana nyingine ujumbe ukiingia sehemu nyingine isipokuwa inbox inakuwa si kawaida. Katika makala hii napenda kukushirikisha hatua unazopaswa kufuata ikiwa utakuta barua pepe imeingia katika sehemu nyingine yoyote badala ya inbox.
(a) Ingia katika akaunti yako ya barua pepe ya Yahoo.
(b) Nenda upande wa kulia juu kuna sehemu ina alama kama ya gia,kisha bofya sehemu iliyoandikwa settings.
(c) Bofya sehemu iliyoandikwa Filters.Katika kiboksi kitakachotokea kunatakiwa kusiwe na kitu chochote.Ikiwa utakuta maandishi yoyote , yachague kwa kubofya maandishi yaliyopo , kisha katika sehemu ya juu bofya sehemu iliyoandikwa Remove
(d) Baada ya hatua (c) bofya kitufe cha Save kilichopo upande wa kushoto chini ili kukamilisha.
Hatua hizi ni kwa ajili ya akaunti za barua pepe za Yahoo tu.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Barua Pepe Kutoingia Katika Inbox
Related Posts:
Aina Tano (05) za Uwekezaji Zinazoweza Kubadili Maisha Yako Ili kuweza kuwa na utajiri endelevu katika maisha yako na unaojitosheleza ni muhimu ukawa mwekezaji. Uwekezaji upo wa aina nyingi. Hapa ninakuletea aina za uwekezaji unazoweza kuzifanya ili kukuwezesha wewe na wale watu wako… Read More
Uchambuzi Kitabu cha " DIFFICULT CONVERSATIONS - HOW TO DISCUSS WHAT MATTERS MOST" Kuna wakati mada ambayo unahitaji kuzungumza na hadhira kuwa na ugumu katika uwasilishaji. Na hii hupelekea kuleta hata hofu kuona kama mahusiano yako na hadhira kuweza kubadilika. Changamoto hii huonekana hasa katika mada … Read More
Hatua Saba (07) za Kukusaidia Kuelekea Uhuru wa Kifedha Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki kila mtu anapenda kuishi katika hali ya kuwa na kiwango cha fedha kinachoweza kuhudumia mahitaji yale ya muhimu na kufanya… Read More
Jinsi ya Kukabili Changamoto za Uandishi Katika Blogu Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Pasipo kutegemea lugha gani unaitumia katika uandishi wa makala ambazo unaziweka katika blogu yako, bado suala la uandishi lina cha… Read More
Uchambuzi wa Kitabu cha " SECRETS OF SELF MADE MILLIONAIRE" Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Mwandishi na mjasiriamali Adam Khoo kupitia kitabu hiki cha Secrets of Self Made Millionare, anatushirikisha mbinu mbalimbali amb… Read More
0 comments:
Post a Comment