Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Partition katika kompyuta ni kitendo cha kugawa hard drive katika sehemu mbalimbali. Kitendo hiki husaidia kutenganisha sehemu ya hard drive ambapo umeweka operating system kutokuchanganyika na sehemu ya hard drive ambayo utakuwa unaweka data zako. Hii inasaidia sana kuzuia data zako kuathiriwa (corrupted).
Makala Inayohusiana :Jinsi ya Kutengeneza Bootable USB Drive
Katika makala hii ninapenda kukushirikisha hatua kwa hatua jinsi unavyoweza kufanya partition ya hard drive katika kompyuta amabayo imekuwa installed Microsoft Windows 7.
(a) Baada ya kuwasha kompyuta yako nenda katika sehemu ya start iliyopo kushoto chini.
(b) Bofya kwa kutumia kitufe cha kulia cha mouse katika neno Computer, kisha tafuta neno Manage na bofya hapo.
(c) Bofya katika neno Disk Management ili uweze kuona hard drive zote ambazo zipo katika kompyuta yako. Angalia iliyoandikwa Disk 0 ndiyo ambayo utaitumia.
(d) Bofya kwa kutumia kitufe cha kulia cha mouse katika hard drive unayohitaji kufanya parrtition na kisha uchague maneno yaliyoandikwa Shrink Volume.
Makala Inayohusiana: Je, Unafahamu Kifaa Kinachoitwa Mouse?
(e) Baada ya hatua (d) bofya neno shrink ili kukamilisha.
(f) Baada ya hatua (e) utapata partition ambayo imeandikwa Unallocated na rangi yake itakuwa nyeusi kwa juu, bofya kwa kitufe cha kulia sehemu hiyo na uchague maneno create new simple volume na unapofika mwisho kabisa utatakiwa kuchagua neno Finish ili kukamilisha hatua zote.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako
Jinsi ya Kufanya Partition Katika Hard Drive
Related Posts:
Zingatia Haya Ili Uifanye Siku Yako BoraMafanikio yako hayatokei siku moja, bali ni muunganiko wa siku nyingi ambazo umeishi kwa mafanikio. Daima usiruhusu watu waiharibu siku yako kwa kuleta matatizo yao katika siku yako kwa njia yoyote mfano kwa kukuudhi. … Read More
Salamu ya Mwezi AprilJambo la kwanza Simamia mawazo na shughuli zako kwa ufanisi wa hali ya juu Jambo la pili Kila unachokifanya kifanye kiwe na muonekano tofauti na ambavyo wengine wamezoea kukifanya kwa kuhakikisha kinaleta manufaa kwako pamoj… Read More
Jambo Moja la Kuzingatia Ili Uwe Tajiri Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE MicrosoftInternetExplorer4 Kabla ya kit… Read More
Kitu Hiki Kimoja Ni Muhimu Kuliko Kiwango Cha Fedha Unachotaka.Inawezekana umefika katika hatua ambayo unaona kama ungekuwa na kiasi fulani cha fedha basi matatizo yako yote ambayo yamekuwa yanakusumbua au yanakukabili bila kujali yana umri kiasi gani yangekuwa yamepatiwa ufumbuzi wa … Read More
Mbinu ya Kuishi Kila SikuAnza na kuimaliza siku vizuri kadiri inavyowezekana Begin and end each day properly… Read More
0 comments:
Post a Comment