Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Partition katika kompyuta ni kitendo cha kugawa hard drive katika sehemu mbalimbali. Kitendo hiki husaidia kutenganisha sehemu ya hard drive ambapo umeweka operating system kutokuchanganyika na sehemu ya hard drive ambayo utakuwa unaweka data zako. Hii inasaidia sana kuzuia data zako kuathiriwa (corrupted).
Makala Inayohusiana :Jinsi ya Kutengeneza Bootable USB Drive
Katika makala hii ninapenda kukushirikisha hatua kwa hatua jinsi unavyoweza kufanya partition ya hard drive katika kompyuta amabayo imekuwa installed Microsoft Windows 7.
(a) Baada ya kuwasha kompyuta yako nenda katika sehemu ya start iliyopo kushoto chini.
(b) Bofya kwa kutumia kitufe cha kulia cha mouse katika neno Computer, kisha tafuta neno Manage na bofya hapo.
(c) Bofya katika neno Disk Management ili uweze kuona hard drive zote ambazo zipo katika kompyuta yako. Angalia iliyoandikwa Disk 0 ndiyo ambayo utaitumia.
(d) Bofya kwa kutumia kitufe cha kulia cha mouse katika hard drive unayohitaji kufanya parrtition na kisha uchague maneno yaliyoandikwa Shrink Volume.
Makala Inayohusiana: Je, Unafahamu Kifaa Kinachoitwa Mouse?
(e) Baada ya hatua (d) bofya neno shrink ili kukamilisha.
(f) Baada ya hatua (e) utapata partition ambayo imeandikwa Unallocated na rangi yake itakuwa nyeusi kwa juu, bofya kwa kitufe cha kulia sehemu hiyo na uchague maneno create new simple volume na unapofika mwisho kabisa utatakiwa kuchagua neno Finish ili kukamilisha hatua zote.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako
Jinsi ya Kufanya Partition Katika Hard Drive
Related Posts:
Jenga Mtazamo Huu Unapouliza MaswaliTukio lolote linapotutokea bila kujali ni zuri au baya katika akili kuna mambo matatu huwa yanaendelea: a) Fikra (thoughts) b) Hisia (feelings) c) Hali (circumstances) Bila kujali hali ya tukio mambo hayo 3 ndiyo yanayotuon… Read More
Fahamu Haya Kama KiongoziKwa kila unayemuongoza unahusiana naye kwa kulingana na mojawapo kati ya ngazi hizi tano. Ngazi ya chini kabisa ni ngazi ya kwanza na ngazi ya juu kabisa ni ngazi ya tano: 1. Ngazi ya kwanza ambayo tunaanza nayo katika safar… Read More
Umakini Unaouhitaji Kabla Hujaanza Kufanya LoloteKutegemeana mtu na mtu kuna tofauti kati ya vitu vinavyoleta bugudha wakati unafanya jambo. Mfano kuna mtu hawezi kufanya kazi katika mazingira yenye kelele au wakati redio inazungumza wakati huo huo kuna mwingine anaweza kuf… Read More
Je, Umepoteza Ujasiri (Confidence)?Katika jambo lolote unalofanya unahitaji kuwa na ujasiri ili uweze kuwa na nguvu au stamina ya kuweza kulileta katika uhasilia(kulikamilisha) bila kujali vikwazo utakavyokutana navyo njiani. Zifuatazo ni njia au namna ambavy… Read More
Unahitaji Wastani wa Maswali 12 KufanikiwaUnapofanya maamuzi ya kutaka kufanikiwa unahitaji kufanya mabadiliko ya msingi (fundamental change).Ili kufanya mabadiliko unahitaji namna nzuri ya kuelewa sehemu ambayo unatakiwa kuanzia. Sehemu iliyo bora kabisa ya kuanza… Read More
0 comments:
Post a Comment