Thursday, 3 November 2016

Jinsi ya Kutatua Tatizo la Barua Pepe Kutoingia Katika Inbox

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Barua pepe ni njia ambayo watumiaji wa kompyuta hutumia kutuma ujumbe kwa njia ya kidigitali. Kuna kampuni za aina mbalimbali ambazo zinatoa huduma hii. Baadhi ya kampuni ni Google, Yahoo na kadhalika. Ili uweze kupokea na kutuma ujumbe kwa njia ya barua pepe ni lazima uwe na akaunti katika kampuni hizi. Akaunti hizi huwa hazihitaji malipo.

Makala Inayohusiana: Faida Nne (04) Unazopata Ukiwa na Akaunti ya Gmail.

Kawaida ujumbe unapoingia katika akaunti yako ya barua pepe unapaswa kukaa katika sehemu inayoitwa inbox. Kwa maana nyingine ujumbe ukiingia sehemu nyingine isipokuwa inbox inakuwa si kawaida. Katika makala hii napenda kukushirikisha hatua unazopaswa kufuata ikiwa utakuta barua pepe imeingia katika sehemu nyingine yoyote badala ya inbox.

(a) Ingia katika akaunti yako ya barua pepe ya Yahoo.

(b) Nenda upande wa kulia juu kuna sehemu ina alama kama ya gia,kisha bofya sehemu iliyoandikwa settings.



(c) Bofya sehemu iliyoandikwa Filters.Katika kiboksi kitakachotokea kunatakiwa kusiwe na kitu chochote.Ikiwa utakuta maandishi yoyote , yachague kwa kubofya maandishi yaliyopo , kisha katika sehemu ya juu bofya sehemu iliyoandikwa Remove



(d) Baada ya hatua (c) bofya kitufe cha Save kilichopo upande wa kushoto chini ili kukamilisha.

Hatua hizi ni kwa ajili ya akaunti za barua pepe za Yahoo tu.

Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako

Wednesday, 2 November 2016

Jinsi ya Kufanya Partition Katika Hard Drive

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Partition katika kompyuta ni kitendo cha kugawa hard drive katika sehemu mbalimbali. Kitendo hiki husaidia kutenganisha sehemu ya hard drive ambapo umeweka operating system kutokuchanganyika na sehemu ya hard drive ambayo utakuwa unaweka data zako. Hii inasaidia sana kuzuia data zako kuathiriwa (corrupted).

Makala Inayohusiana :Jinsi ya Kutengeneza Bootable USB Drive

Katika makala hii ninapenda kukushirikisha hatua kwa hatua jinsi unavyoweza kufanya partition ya hard drive katika kompyuta amabayo imekuwa installed Microsoft Windows 7.

(a) Baada ya kuwasha kompyuta yako nenda katika sehemu ya start iliyopo kushoto chini.





(b) Bofya kwa kutumia kitufe cha kulia cha mouse katika neno Computer, kisha tafuta neno Manage na bofya hapo.



(c) Bofya katika neno Disk Management ili uweze kuona hard drive zote ambazo zipo katika kompyuta yako. Angalia iliyoandikwa Disk 0 ndiyo ambayo utaitumia.



(d) Bofya kwa kutumia kitufe cha kulia cha mouse katika hard drive unayohitaji kufanya parrtition na kisha uchague maneno yaliyoandikwa Shrink Volume.



Makala InayohusianaJe, Unafahamu Kifaa Kinachoitwa Mouse?

(e) Baada ya hatua (d) bofya neno shrink ili kukamilisha.

(f) Baada ya hatua (e) utapata partition ambayo imeandikwa Unallocated na rangi yake itakuwa nyeusi kwa juu, bofya kwa kitufe cha kulia sehemu hiyo na uchague maneno create new simple volume na unapofika mwisho kabisa utatakiwa kuchagua neno Finish  ili kukamilisha hatua zote.




















Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako

Tuesday, 1 November 2016

Mfumo Pekee Utakakokusaidia Kukidhi Mahitaji ya Mteja

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Suala la kukidhi mahitaji ya mteja unaowahudumia linakwenda sambamba na utoaji wa huduma bora kwa mteja. Kiwango cha kukidhi mahitaji ya mteja hupimwa na jinsi unavyoweza kutimiza mahitaji ya mteja kuzidi ahadi uliyompa kabla hujampatia huduma.


Rafiki usipende kukisia au kuhisi matarajio ya mteja kupitia huduma unayotoa, unahitaji kujifunza kumuuliza mteja kuhusu matarajio yake. Jambo lingine ni kuwa matarajio ya mteja huwa yanabadilika mara kwa mara na yataendelea kuwa yanabadilika, hivyo unahitaji kutambua au kuyajua matarajio haya katika hali ya uendelevu (on-going basis).
Katika makala hii ninapenda kukushirikisha mambo machache ambayo yatakusaidia kuhakikisha unakidhi mahitaji na matarajio ya mteja kupitia huduma anyaopokea kutoka kwako.
(a) Tambua mahitaji ya mteja
Ikiwa kama hutambui mahitaji ya mteja wako ni vigumu sana kumridhisha au kukidhi matarajio yake anapopokea huduma yako. Kuna njia mbalimbali zinazoweza kukusaidia kutambua mahitaji ya mteja wako. Baadhi ya njia ni malalamiko kutoka kwa mteja , mrejesho kutokana na matumizi ya huduma yako, hoja mbalimbali (query) na tafiti.
(b) Jibu mahitaji ya mteja
Baada ya kutambua mahitaji ya mteja hatua inayofuata ni muhimu kuhakikisha unakidhi au unajibu mahitaji ya mteja. Kutegemeana na njia iliyotumika kutambua mahitaji ni muhimu kukawekwa mkakati sambamba ambao utajibu mahitaji husika. Ni muhimu pia kuwa na utaratibu ambao uko wazi unaoweza kupimika hata kwa wasaidizi wako , mfano ni muda ambao utachukua kutoka ulipopewa malalamiko na mteja mpaka muda ambapo umemjibu.
(c) Utunzaji wa kumbukumbu
Ni muhimu kuwa na mfumo ambao utahifadhi au utarekodi mahitaji ambayo yamepokewa kutoka kwa mteja, na majibu ambayo amepatiwa mteja. Hii itakusaidia kuwa na taarifa muhimu ambazo zinaweza zikatumika muda wowote. Pia itakusaidia katika tathmini ya jinsi unavyokidhi mahitaji ya mteja wako na uwekaji wa utaratibu mzuri utakaosaidia kuoanisha aina ya mahitaji kutoka kwa mteja na uwezo wa wasaidizi wako ambao wanaweza kujibu vizuri mahitaji hayo.
Kwa kuzingatia mambo hayo niliyoyaeleza hapo juu, huduma yako itaendelea kuwa hai au kudumu au kuwa endelevu (sustainable).
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako

Monday, 31 October 2016

Kanuni Kumi (10) za Huduma Bora Kwa Mteja

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Tafiti zinaonesha asilimia sabini ya sababu zinazosababisha kampuni kupoteza wateja zinahusiana kwa kiwango kidogo sana na bidhaa. Ila sababu kubwa ni kila kitu kinachohusiana na huduma kwa mteja. Katika makala ya leo napenda kukushirikisha kanuni kumi zitakazokuongoza katika kutoa huduma bora kwa wateja:



(a) Wateja utawapata ikiwa utazalisha bidhaa au utatoa huduma zenye ubora wa hali ya juu, na wateja ambao umewapata wataendelea kutumia bidhaa au huduma yako ikiwa utakuwa na kiwango cha juu cha huduma kwa mteja (superior customer service).
(b) Unalo jukumu la kuhakikisha unajibu mahitaji na matarajio ya wateja wako kadiri inavyowezekana. Wateja wanahitaji kuridhishwa kwa kuondolewa hofu walizonazo na kutatua malalamiko yao kuhusu bidhaa au huduma yako.
(c) Wateja ndiyo kiungo muhimu cha uhai wa kampuni yako. Uwepo wa wateja ndiyo unaosababisha kampuni yako iweze kuendelea kuwepo.
(d) Wateja ni binadamu kama wewe, wana hisia, wanafurahi, wanachukia kama ambavyo kwa upande wako ingekuwa, hivyo ni muhimu mara zote kuhakikisha unawahudumia vizuri zaidi kuliko ambavyo ungependa kuhudumiwa.
(e) Wateja wana haki ya kupokea huduma bora na kupewa umakini wakati unawapatia huduma.
(f) Wateja wanakupendelea kwa kutembelea kampuni yako na haina maana kuwa wewe ndiye unawapendelea kwa kuwahudumia bali wanafanya biashara yako iendelee kukua.
(g) Lengo kuu la bidhaa unayozalisha au huduma unayotoa ni wateja unaowahudumia na siyo vinginevyo.
(h) Wateja hawakutegemei wewe bali wewe ndiye unawategemea ili biashara yako iendelee kuwepo. Hakuna kitu ambacho mteja anapoteza kama hatatumia bidhaa au huduma yako.
(i) Mwajiri au bosi wako mkuu ni mteja unayemhudumia.
(j) Ubora  wa huduma ndiyo silaha pekee ambayo itakusaidia kutangaza bidhaa au huduma yako na inasaidia kuendesha biashara yako.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako

Saturday, 29 October 2016

Namna Bora ya Kuandika Kichwa cha Habari (Title) Katika Makala

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Rafiki katika moja ya makala zilizopita nilikushirikisha kuhusu jinsi ya kukabili changamoto za uandishi katika blogu .Katika hiyo makala nilieleza kwa undani mambo makuu matatu; jambo la kwanza ni kusoma vitabu, jambo la pili ni kuandika kila siku na jambo la tatu ni kufanya tathmini ya makala unazoandika. Kama hujasoma makala hiyo unaweza kubonyeza maandishi hapa chini kufungua usome kabla hujaendelea.



Katika makala hii ninapenda kukushirikisha changamoto nyingine inayohusiana na kichwa cha habari (title) cha makala husika katika blogu yako.
Kichwa cha habari cha makala ndicho kinachobeba ujumbe mkuu katika makala yako. Kichwa hiki ni muhimu kiwe na sifa zifuatazo:
(a) Kiwe na maneno machache (kifupi) kadiri inavyowezekana.
(b) Kiwe kinavutia au kumhamasisha msomaji kuweza kufungua na kuangalia maarifa yaliyobebwa na kichwa husika.
(c) Kiwe na muundo wa herufi ya kwanza ya kila neno kuwa herufi kubwa.
Faida kubwa unazozipata kwa kichwa cha habari kuwa na sifa hizo ni:
(a) Kupata wasomaji wengi ambao watakuwa wanakufuatilia.
(b) Kuonesha kiwango cha umakini katika uandishi wako.
Kuna njia mbili unazoweza kutumia kuandika kichwa cha habari bora, kifupi na kinachovutia au kuhamasisha wasomaji wako.
(a) Njia ya kwanza ni kuanza kuandika ujumbe na kumaliza na kichwa cha habari.
Katika njia hii unaandika makala yako yote ukiwa umeipangilia kuwa na sehemu kuu tatu; utangulizi (introduction), mada kuu (body) na hitimisho (conclusion).
Baada ya kukamilisha kuandika sehemu zote hizo tatu, unaipitia na kuanza kutafakari maneno machache ambayo yanaweza kubeba ujumbe wote ulioandika.
Faida ya njia hii ni kuwa haikubani wakati wa uandishi kuwa ni mambo gani uyaandike kutokana na kuwa haujaanza na kichwa cha habari ambacho kingekupa mipaka ya vitu gani vya kuandika. Kwa hiyo unakuwa huru zaidi kuweka mawazo na maarifa yako yote kuhusu mada unayoandika.
(b) Njia ya pili ni kuanza kuandika kichwa cha habari na kumaliza na ujumbe.
Njia hii ipo kinyume cha njia (a) niliyoeleza hapo juu. Hapa unaanza na kichwa cha habari ambacho kinakupa mipaka ya vitu vya kuandika maana unakuwa tayari umeshaweka mwongozo. Ni njia ambayo unahitaji kuweka jitihada sana ili kichwa cha habari kiweze kuendana na ujumbe uliomo ndani.
Pamoja na hiyo changamoto rafiki napenda nikushirikishe kifaa cha mtandaoni ambacho kinaweza kukusaidia kupata kichwa cha habari  kizuri na kinachovutia. Nenda katika Google tafuta Portent Content Idea Generator . Ukishafungua tovuti yao unaweza kuweka mada na ukawa unabofya kupata vichwa mbalimbali.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Friday, 28 October 2016

Jinsi ya Kupata na Kuongeza Wasomaji Katika Blogu Yako

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Rafiki katika moja ya makala zilizopita nilikushirikisha kuhusu hatua nne ambazo zinafuatwa katika uandishi wa makala katika blogu. Moja ya hatua ambayo niliandika ni kuhusu kuhamasisha. Kama hujasoma makala hiyo unaweza kubonyeza maandishi hapa chini kufungua usome kabla hujaendelea.


Katika makala ya leo napenda kukushirikisha namna ya kuangalia chanzo (source) wanapotokea wasomaji wanaotembelea blogu yako. Hapa nitaeleza namna ya kusoma hizi takwimu kisha nitaeleza namna ya kupata maana au tafsiri kutoka katika takwimu.



(a) Ingia katika Dashboard yako ya blogger, kisha bofya jina la blogu yako
(b) Nenda upande wa kushoto na bofya sehemu iliyoandikwa maneno Stats. Mara baada ya kubofya chini yake yatatokea maneno yafuatayo; Overview, Posts, Traffic Sources na Audiences.
(c) Bofya sehemu iliyoandikwa maneno Traffic Sources. Sehemu hii imegawanyika katika sehemu tatu. Sehemu ya kwanza ni referring URLs, sehemu ya pili ni referring sites na sehemu ya tatu ni search keywords.
Katika sehemu ya URLs na sites wataorodhesha tovuti ambazo wasomaji wako walipata link ya makala kutoka katika blogu. Mfano m.facebook.com hii ina maana msomaji alitokea katika mtandao wa facebook kabla ya kufika katika tovuti yako.
Katika sehemu ya search keywords hii inaonesha msomaji wako alitafuta neno gani katika Google kabla ya kubofya link ya makala yako na kuisoma ikiwa ni mojawapo ya majibu ya maneno aliyoyatafuta.
Hizi sehemu zote tatu zitaorodheshwa na kupangiliwa kuanzia ambayo wasomaji wengi wameitumia yaani yenye click nyingi na kuendelea mpaka yenye click chache.
Mathalani kama Facebook ndiyo imeonekana ina namba kubwa kuliko mtandao mwingine kati ya ile iliyoorodheshwa. Hii ina maana Facebook ni sehemu ambayo unahitaji kuipa kipaumbele katika kuwafikia wasomaji wako kupitia vile unavyovihitaji katika blogu. Lakini pia kwa mitandao mingine unahitaji kuweka jitihada uweze kupata pia wasomaji au kuamua kuacha mitandao mingine ili kuwekeza nguvu zote katika mtandao wa facebook ambao umekuonyesha una wasomaji wengi.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako

Thursday, 27 October 2016

Jinsi ya Kutatua Ukosefu wa Intaneti Katika Smartphone

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Rafiki kuna wakati unakuta katika smartphone yako umeweka kifurushi cha kutosha cha intaneti lakini huwezi kutumia kutokana na kuikosa. Changamoto hii husababishwa na settings za Access Point Name (APN) kuwa tofauti na zile ambazo zimetolewa na mtoa huduma.
APN ni jina ambalo mtoa huduma wa mtandao wa simu analitumia kuunganisha kati yake na mtandao mwingine wa intaneti. Hii ni kwa ajili ya kuwapatia watumiaji wa mtandao wa simu huduma ya intaneti katika simu zake.



Katika makala hii napenda kukushirikisha hatua unazohitaji kuzifuata ili kufanya settings za APN katika smartphone yako.
(a) Bofya sehemu ya settings katika smartphone yako
(b) Tafuta sehemu iliyoandikwa network au wireless & network, kisha bofya sehemu iliyoandikwa more
(c) Mara baada ya kufunguka, bofya sehemu iliyoandikwa Mobile Networks
(d) Tafuta na bofya sehemu iliyoandikwa Access Point Names
(e) Ikiwa kuna APN yoyote ambayo ilishafanyiwa settings itaonekana na jina lake. Ili kufanya settings sahihi, bofya hilo jina la APN.
(f) Utahitajika kubofya kwa kuanza sehemu iliyoandikwa Name na andika maneno yafuatayo:
i . Kama unatumia mtandao wa Vodacom andika Vodacom
ii . Kama unatumia mtandao wa Tigo andika Tigo
iii . Kama unatumia mtandao wa Halotel andika halotel
iv . Kama unatumia mtandao wa Airtel andika Tz-airtelweb
v . Kama unatumia mtandao wa Zantel andika zantel
(g) Baada ya hatua (f) bofya sehemu iliyoandikwa APN na andika maneno yafuatayo:
i . Kama unatumia mtandao wa Vodacom andika internet
ii . Kama unatumia mtandao wa Tigo andika tigoweb
iii . Kama unatumia mtandao wa Halotel andika b-internet
iv . Kama unatumia mtandao wa Airtel andika internet
v . Kama unatumia mtandao wa Zantel andika znet
(h) Baada ya hatua (g) bofya katika vidoti vitatu kulia juu , kisha chagua na kubofya neno save ili kukamilisha settings. Hakikisha pia umeweka on Mobile Data.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako