Thursday, 27 October 2016

Jinsi ya Kutatua Ukosefu wa Intaneti Katika Smartphone

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Rafiki kuna wakati unakuta katika smartphone yako umeweka kifurushi cha kutosha cha intaneti lakini huwezi kutumia kutokana na kuikosa. Changamoto hii husababishwa na settings za Access Point Name (APN) kuwa tofauti na zile ambazo zimetolewa na mtoa huduma.
APN ni jina ambalo mtoa huduma wa mtandao wa simu analitumia kuunganisha kati yake na mtandao mwingine wa intaneti. Hii ni kwa ajili ya kuwapatia watumiaji wa mtandao wa simu huduma ya intaneti katika simu zake.



Katika makala hii napenda kukushirikisha hatua unazohitaji kuzifuata ili kufanya settings za APN katika smartphone yako.
(a) Bofya sehemu ya settings katika smartphone yako
(b) Tafuta sehemu iliyoandikwa network au wireless & network, kisha bofya sehemu iliyoandikwa more
(c) Mara baada ya kufunguka, bofya sehemu iliyoandikwa Mobile Networks
(d) Tafuta na bofya sehemu iliyoandikwa Access Point Names
(e) Ikiwa kuna APN yoyote ambayo ilishafanyiwa settings itaonekana na jina lake. Ili kufanya settings sahihi, bofya hilo jina la APN.
(f) Utahitajika kubofya kwa kuanza sehemu iliyoandikwa Name na andika maneno yafuatayo:
i . Kama unatumia mtandao wa Vodacom andika Vodacom
ii . Kama unatumia mtandao wa Tigo andika Tigo
iii . Kama unatumia mtandao wa Halotel andika halotel
iv . Kama unatumia mtandao wa Airtel andika Tz-airtelweb
v . Kama unatumia mtandao wa Zantel andika zantel
(g) Baada ya hatua (f) bofya sehemu iliyoandikwa APN na andika maneno yafuatayo:
i . Kama unatumia mtandao wa Vodacom andika internet
ii . Kama unatumia mtandao wa Tigo andika tigoweb
iii . Kama unatumia mtandao wa Halotel andika b-internet
iv . Kama unatumia mtandao wa Airtel andika internet
v . Kama unatumia mtandao wa Zantel andika znet
(h) Baada ya hatua (g) bofya katika vidoti vitatu kulia juu , kisha chagua na kubofya neno save ili kukamilisha settings. Hakikisha pia umeweka on Mobile Data.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako

Related Posts:

  • Kwa Nini Unahitaji Kujifunza Jambo Jipya Kila Siku?Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki mabadiliko na ukuaji ni vitu viwili muhimu vyenye mchango mkubwa katika maisha tunayoishi kila siku. Maisha yanakua na ladha a… Read More
  • Uchambuzi Kitabu cha " MEGALIVING, 30 DAYS TO PERFECT LIFE"Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Robin Sharma ni mwandishi wa kitabu cha MEGALIVING, 30 DAYS TO PERFECT LIFE. Katika kibao hiki Robin anaeleza namna ambavyo unaweza k… Read More
  • Njia Bora Ya Kukabili Changamoto YoyoteHabari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki maisha tunayoishi yana changamoto za aina mbalimbali. Changamoto hizi ni njia pekee ambayo kama utaiitumia vizuri itakusaidia … Read More
  • Uchambuzi Kitabu cha " THE COMPOUND EFFECT"Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Darren Hardy ni mwandishi wa kitabu cha THE COMPOUND EFFECT. Katika kitabu hiki mwandishi anatueleza siri kubwa iliyopo katika kufany… Read More
  • Namna Ya Kudelete File Katika KompyutaHabari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki moja ya operation ambayo inafanyika mara kwa mara katika matumizi ya kompyuta ni delete. Delete hufanya kazi ya kufuta file li… Read More

0 comments:

Post a Comment