Friday, 28 October 2016

Jinsi ya Kupata na Kuongeza Wasomaji Katika Blogu Yako

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Rafiki katika moja ya makala zilizopita nilikushirikisha kuhusu hatua nne ambazo zinafuatwa katika uandishi wa makala katika blogu. Moja ya hatua ambayo niliandika ni kuhusu kuhamasisha. Kama hujasoma makala hiyo unaweza kubonyeza maandishi hapa chini kufungua usome kabla hujaendelea.


Katika makala ya leo napenda kukushirikisha namna ya kuangalia chanzo (source) wanapotokea wasomaji wanaotembelea blogu yako. Hapa nitaeleza namna ya kusoma hizi takwimu kisha nitaeleza namna ya kupata maana au tafsiri kutoka katika takwimu.



(a) Ingia katika Dashboard yako ya blogger, kisha bofya jina la blogu yako
(b) Nenda upande wa kushoto na bofya sehemu iliyoandikwa maneno Stats. Mara baada ya kubofya chini yake yatatokea maneno yafuatayo; Overview, Posts, Traffic Sources na Audiences.
(c) Bofya sehemu iliyoandikwa maneno Traffic Sources. Sehemu hii imegawanyika katika sehemu tatu. Sehemu ya kwanza ni referring URLs, sehemu ya pili ni referring sites na sehemu ya tatu ni search keywords.
Katika sehemu ya URLs na sites wataorodhesha tovuti ambazo wasomaji wako walipata link ya makala kutoka katika blogu. Mfano m.facebook.com hii ina maana msomaji alitokea katika mtandao wa facebook kabla ya kufika katika tovuti yako.
Katika sehemu ya search keywords hii inaonesha msomaji wako alitafuta neno gani katika Google kabla ya kubofya link ya makala yako na kuisoma ikiwa ni mojawapo ya majibu ya maneno aliyoyatafuta.
Hizi sehemu zote tatu zitaorodheshwa na kupangiliwa kuanzia ambayo wasomaji wengi wameitumia yaani yenye click nyingi na kuendelea mpaka yenye click chache.
Mathalani kama Facebook ndiyo imeonekana ina namba kubwa kuliko mtandao mwingine kati ya ile iliyoorodheshwa. Hii ina maana Facebook ni sehemu ambayo unahitaji kuipa kipaumbele katika kuwafikia wasomaji wako kupitia vile unavyovihitaji katika blogu. Lakini pia kwa mitandao mingine unahitaji kuweka jitihada uweze kupata pia wasomaji au kuamua kuacha mitandao mingine ili kuwekeza nguvu zote katika mtandao wa facebook ambao umekuonyesha una wasomaji wengi.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako

Related Posts:

  • Je, Umepoteza Ujasiri (Confidence)?Katika jambo lolote unalofanya unahitaji kuwa na ujasiri ili uweze kuwa na nguvu au stamina ya kuweza kulileta katika uhasilia(kulikamilisha) bila kujali vikwazo utakavyokutana navyo njiani. Zifuatazo ni njia au namna ambavy… Read More
  • Kanuni Inayoamua Wewe Kufanikiwa au KushindwaKatika mambo tunayofanya kuna matokeo mawili; aidha kufanikiwa sawasawa na malengo tuliyojiwekea kabla hatujanza kutekeleza jambo au kutokufanikiwa ambapo tunaweza kukuita kushindwa kutokana na kutofikia vigezo tulivyoviweka … Read More
  • Fahamu Haya Kama KiongoziKwa kila unayemuongoza unahusiana naye kwa kulingana na mojawapo kati ya ngazi hizi tano. Ngazi ya chini kabisa ni ngazi ya kwanza na ngazi ya juu kabisa ni ngazi ya tano: 1. Ngazi ya kwanza ambayo tunaanza nayo katika safar… Read More
  • Sumu ya MafanikioUnapokosa lengo kubwa katika maisha yako kwa kutokujua nini hasa unahitaji na unakipataje, mara nyingi hupelekea kutegemea maoni au ushauri wa watu wengine zaidi katika kuamua kitu cha kufanya kwa ajili ya maisha yako badala … Read More
  • Mbinu za Kustahimili MatatizoSiri moja kubwa ambayo imewafanya watu waliofanikiwa kuendelea vizuri ni mtazamo juu ya matatizo wanayokutana nayo. Ukizielewa kanuni hizi 6 kuhusu matatizo na kuzifanyia kazi ipasavyo wewe pia utakuwa mshindi. 1. Kila mtu a… Read More

0 comments:

Post a Comment