Thursday 2 July 2015

Jinsi ya Kuwaandaa Kuongoza Viongozi Watarajiwa (Chipukizi)

Habari na karibu ndugu mpenzi msomaji wa blogu hii ya. Ni matumaini yetu umekuwa na wiki ya mafanikio sana.


Leo nitazungumzia namna ya kuwaandaa watu wenye sifa za uongozi ambao umewatambua upo nao katika timu yako katika taasisi. Kuwaandaa viongozi hawa watarajiwa kunahusisha wewe ambaye tayari ni kiongozi pamoja na hao viongozi watarajiwa , nah ii inaweza kulinganishwa kwa kiasi Fulani kama unawawapatia mafunzo.

  1. Tengeneza Mahusiano na Viongozi Chipukizi Unaowaandaa
Viongozi chipukizi ambao umeshawatambua unahitaji kuwafahamu, kuwasikiliza historia za maisha yao ili uweze kuwajua zaidi ya vile unavowajua tu kiofisi. Huhitaji kujua kuhusu uwezo au ubora wao tu bali unahitaji pia kujua kuhusu madhaifu yao pia ili uweze kujua namna ya kuwafanya wakamilifu kwa hayo mapungufu uliyoyatambua. Na ukiweza kujenga mahusiano mazuri maanake utafanya wakupende na pia kuongeza nia na kiu kwao kujifunza kutoka kwako

  1. Washirikishe ndoto yako
Wakati unaendelea kuwafahamu usiwaache wao peke yao tu wakuambie ya kwao, na wewe pia unahitaji kuwashirikisha pi historia ya maisha yako na unahitaji kwenda hatua ya ziada kwa kuwashirikisha ndoto yako kuhusiana na taasisi ambayo unaiongoza. Na hii itawasaidia kujua ni wapi unataka kwenda na hivo kujiunga kujitoa kufuatana nawe mpaka mwisho wa safari yako

  1. Waombe utayari wao kujitoa kiuongozi
Moja ya kiungo muhimu ambacho kinaweza kumfanya kiongozi chipukizi kuwa kiongozi mwenye mafanikio, ni utayari wa kujitolea kiuongozi. Ni muhimu sana kwa hawa viongozi chipukizi unaowaandaa wawe wamejitoa kwa ajili ya uongozi pamoja na taasisi. Na unahitaji kuwaeleza gharama ambayo itawachukua kwa wao kuwa viongozi, na jambo la muhimu ni uwe mkweli kuhusu mambo ambayo watahitaji kuzingatia au kuyajua hata kabla ya hatua yenyewe ya kufanya maamuzi ya kukubali kuweza kujitoa kiuongozi.

  1. Weka malengo kwa ajili ya ukuaji
Viongozi hawa chipukizi wanahitaji kujua malengo yaliyo fasaha ambayo wanatakiwa kuyapigania au kuyafanikisha, nah ii itawasaidia kujua ni nini wnatakiwa kufanya na pia ni vitu gani vinatarajiwa kutoka kwao. Jambo muhimu zaid la kuzingatia ni unapoweka malengo zingatia malengo yawe yako wazi, fasaha na yanayoeleweka. Malengo yawe ni sahihi kwao lakini pia yawe yanaweza kupimika. Baada ya kuyafahamu hayo malengo ni vizuri yawekwe katika maadnishi ili kila mmoja aweze kujitoa kikamilifu katika malengo hayo

  1. Weka mambo ya msingi sawa
Ni muhimu sana kuweka misingi kwa kuwaelewesha majukumu yao na wayafahamu kwa undani. Weka kwa ufasaha mategemeo yako kwao lakini pia na wao wajue vipaumbele ni vipi katika majukumu yao. Na uhakikishe wanaweza kujua tofauti kati ya kazi iliyo ya umuhimu sana na ile kazi yenye umuhimu kiasi.

  1. Mfumo wa ufundishaji unaofaa
Kuna hatua tano muhimu zinazoweza kukupatia matokeo mazuri hasa inapohusisha kuwaandaa kiuongozi viongozi chipukizi
                                i.            Kuwa mfano kwanza kwa kila unachotaka waweze kukifanya
                              ii.            Wafundishi au waelekeze
                            iii.            Simamia maendeleo ya kile unachowaelekeza
                            iv.            Wahamasishe
                              v.            Wape fursa pia ya kutengeneza viongozi kati yao viongozi chipukizi

  1. Simamia maendeleo yao bila kuacha
Ni muhimu ukawa na mikutano iliyo rasmi na isiyo rasmi pia ili kuweza kujua mahitaji, matatizo ambayo wanakumbana nayo pia. Na hii itakusaidia kuwapatia vifaa sahihi zaidi na kuendelea kuwapa ujasiri na kuwahamasisha.

0 comments:

Post a Comment