Sunday, 9 October 2016

Faida Nne (04) Unazopata Ukiwa na Akaunti ya Gmail.

Habari rafiki yangu unayefuatilia makala zinazowekwa katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Leo napenda kukuletea mambo manne (04) ambayo unaweza kuyafanya kwa kuwa na akaunti ya barua pepe kutoka kampuni ya Google. Akaunti hii hufahamika kwa jina la Gmail.

1. Nafasi ya ukubwa wa kiasi cha Gigabyte 15 kwa ajili ya kuhifadhi taarifa zako mtandaoni
Kila mtu ambaye ana akaunti ya Gmail anapata sehemu ya kuhifadhi "data" yenye ukubwa wa kiasi cha Gigabyte 15. Hii nafasi inapatikana bure bila malipo yoyote. Na unaweza kuzitumia taarifa zako sehemu yoyote duniani ambapo umeunganishwa na mtandao.

2. Kuhifadhi orodha ya majina kutoka katika kumbukumbu ya simu yako
Kila mtu ambaye ana akaunti ya Gmail anapata nafasi ya kuhifadhi majina, namba za simu kutoka katika kumbukumbu ya mawasiliano ya simu husika. Hii huduma pia inapatikana bila ya malipo yoyote. Ni huduma ambayo huwa inasaidia sana wakati aidha unapotaka kubadili simu yako ama simu inapokuwa imeharibika ama simu imepotea. Ikiwa umehifadhi orodha yako katika Gmail utaweza kurejesha orodha ya majina na namba za simu kwa haraka na urahisi.

3. Kuwa na blogu katika mtandao wa blogspot.com
Kila mtu ambaye ana akaunti ya Gmail anaweza kufungua blogu ambapo ataweza kuweka taarifa au maarifa mbalimbali kwenda kwa jamii husika. Blogu hii ataifungua bila ya malipo yoyote. Jina lake la blogu atalipendekeza kutegemeana na anavyoona inafaa na baada ya jina hilo ambalo amependekeza litafuata neno .blogspot.com

4. Kuweka programu mbalimbali katika simu zinazotumia Google Android OS
Programu mbalimbali ambazo zinatumika katika smartphone unaweza kuzipata kutoka katika Play Store. Ili uweze kuziona na kuchagua programu hizi kutoka play store unahitaji kuwa na akaunti ya Gmail. Mfano tunapowapelekea mafundi wa simu watuwekee programu kama vile WhatsApp, You tube, Facebook na kadhalika, wanachofanya hasa ni kutumia akaunti ya Gmail kuingia playstore, kutafuta programu ulizomwambia na kuziweka, ambapo ni kitendo ungeweza pia kukifanya ikiwa unayo akaunti ya Gmail.
Endelea kutembelea mtandao huu kujifunza zaidi.

Related Posts:

  • Fanya Haya ili Ukue1. Usitamani mambo yangekuwa marahisi, tamani ungekuwa bora mno Don't wish it were easier; wish you were better 2. Usitamani ungekutana au ungekuwa na matatizo machache,tamani ungekuwa na ujuzi zaidi Don't wish for less prob… Read More
  • Usifanye Kosa Hili Katika BiasharaUnapoamua kuchagua kuwa utashirikiana na mtu mwingine kufanya biashara ya ndoto yako, usitumie kigezo cha huyo mshirika kuwa ni mmoja wa wanafamilia wako au ni mmoja wa marafiki zako wa karibu sana, utakuwa umejiingiza katika… Read More
  • Tazama Kushindwa kwa Jicho HiliKushindwa hakuamaanishi wewe ndiye uliyeshindwa bali kunamaanisha hujafanikiwa bado Kushindwa hakumaanishi haukutimiza/haujafanikisha kitu bali kunamaanisha umejifunza kitu Kushindwa hakumaanishi wewe ni mjinga bali kunamaa… Read More
  • Je, Unajua?Ni bora kufanya kitu kisicho kamili kuliko kutokufanya chochote kisicho na dosari Better to do something imperfectly than to do nothing flawlessly… Read More
  • Usipuuze TatizoMatatizo mengi kamwe hayatatuliwi au hayadhibiti kwa ufanisi kutokana na kutoyapa uzito wa kutosheleza. Hakuna tatizo ambalo halina umuhimu kiasi kuwa hatuhitaji kujali kuhusu hilo tatizo. Mfano kwa mwanafunzi inawezekena hap… Read More

0 comments:

Post a Comment