Friday, 14 October 2016

Hatua Saba (07) za Kukusaidia Kuelekea Uhuru wa Kifedha

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Rafiki kila mtu anapenda kuishi katika hali ya kuwa na kiwango cha fedha kinachoweza kuhudumia mahitaji yale ya muhimu na kufanya mambo mengine ya ziada. Asilimia kubwa ya watu wanatumia muda na nguvu ili kupata kipato kinachowasaidia kujikimu. Hivyo utakubaliana na mimi hawana uhuru katika maisha yao maana kuna muda fulani maalum lazima awepo kwa mwajiri wake,wanabadilishana muda na ujuzi wake kwa fedha (mshahara). Hapa chini nakushirikisha hatua chache ambazo ukizifanyia kazi zitakusaidia kufikia uhuru wa kifedha.




(a) Kuwa na mtazamo wa kimilionea
Mtazamo huu utakusaidia sana kuyaangalia mambo mbalimbali kwa jicho la tofauti sana. Sehemu ambapo watu wanalalamika kuhusu tatizo wewe utakuwa unaona fursa ya kutengeneza kipato kupitia kutatua tatizo husika. Na mabadiliko haya yatakwenda hadi katika ngazi ya tabia yako, kujifunza kwako, kufikiri kwako. Utakuwa ni mtu ambaye anatatua matatizo na kulipwa kutokana na kuleta suluhisho la tatizo.
(b) Weka kwa ufasaha malengo yako ya kifedha
Suala la kuwa tajiri halitokei kwa bahati mbaya , ni jambo ambalo linatokea kwa maksudi kabisa kutokana na uamuzi wako wa kuwa tajiri. Ufasaha wa malengo unaonekana katika kiwango sahihi unachokitaka kukipata, kiwango hiki ni lazima kiwe kinaweza kupimika. Malengo yanayowezekana kupimika yanasaidia sana katika upangaji wa mkakati, kuonesha kiwango cha jitihada kinachohitajika kuwekwa na pia kukupatia hamasa inayoweza kukupa stamina ya kuweza kupambana hata mambo yanapokuwa magumu.
(c) Tengeneza mpango wa kifedha
Baada ya kukamilisha uwekaji wa malengo, ni muhimu kuwa na mpango wa kukuwezesha kufikia malengo yako. Mpango wako ni lazima uwe na ufasaha ukiwa na maelezo yanayogusa masuala kama vile; kiasi gani utakitunza, kiasi gani utawekeza, idadi ya mifereji ya kipato utakayoitengeneza, kiwango cha faida unachokitaka kutoka katika uwekezaji unaofanya. Ingawa kuna wataalamu ambao wanaweza kukusaidia kutengeneza mpango huu ila ni muhimu suala hili ukalifanya wewe mwenyewe binafsi, hii ni kwa sababu wewe ndiye unayefahamu kwa ufasaha unachokitaka.
(d) Ongeza kiasi chako cha kipato
Kikawaida baada ya kuwa na mpango utaona kama itakuchukua muda mrefu mpaka uweze kufikia uhuru wa kifedha hasa ukifanya ulinganisho na hali yako ya kifedha ya sasa. Ukweli ni kuwa unahitaji kuongeza kipato chako sio kwa kiwango cha asilimia bali ni kiwango cha maradufu, mara tatu au mara nyingi zaidi kadiri inavyowezekana. Ukomo wa kiasi gani ni mara ngapi unaweza kuongeza kipato chako unaamuliwa na uwezo wako hakuna mtu anayeweza kujizuia. Na hili unaweza kulifanya bila kuacha ajira unayofanya au kuhatarisha kwa kuwekeza fedha zote unazopata kwenda katika biashara.
(e) Dhibiti mapato na matumizi yako
Ni muhimu kuangalia mlinganyo kati ya fedha unazoingiza na fedha unazozitoa. Kuingiza fedha nyingi na kuwa na matumizi ya fedha kidogo ndiyo siri kuu. Unapokuwa na matumizi kidogo inasaidia kubakia na kiasi cha fedha ambacho unaweza kuwekeza na kuhifadhi. Tofauti katika maisha ya tajiri na maskini imejengwa hapa  unafanya nini na hiki kiasi kinachobaki.
(f) Kuza fedha ziweze kukurudia katika kiwango cha milioni au zaidi
Baada ya kudhibiti matumizi yako ni vizuri kiasi kile ambacho unabakiza ukiwekeze katika maeneo ambayo faida yake utaipata katika kiwango cha milioni au zaidi. Na siyo unawekeza tuu bila kuzingatia kiwango cha faida unayopata. Hii ni muhimu sababu itafika wakati huwezi kutumia nguvu zako kutengeneza fedha bali fedha uliyonayo iwe inafanya kazi ya kukutengenezea fedha.
(g) Weka ulinzi katika utajiri wako
Utengenezaji utajiri ni suala ambalo utatumia muda na jitihada. Ni muhimu kuhakikisha haupati hasara katika uwekezaji ambao umefanya. Ulinzi unautengeneza kwa kuweka bima , kumpata mtaalamu wa kisheria ambaye anaweza kukushauri mambo ya kisheria kuhusu uwekezaji unaoufanya, na hata wataalamu wa mahesabu ya fedha ili wakuongoze katika eneo hilo bila ya kupata hasara.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Related Posts:

  • Msingi wa kutimiza maisha yenye ufanisiUwezo uliopo ndani yetu ni mkubwa sana kuliko kile ambacho tumeshakitendea haki kwa nafasi zetu tulizonazo kwa kutendea ulimwengu. Maswali haya yatakusaidia kutafakari kitu gani ambacho unacho ndani yako bado hujakileta ulimw… Read More
  • Njia Rahisi Kuzuia Utendaji MbovuKama hali yetu ya hamasa ya kufanya jambo fulani haifanani/haiendani na jambo tunalohitajika kulifanya, moja kwa moja inapelekea kukosa hamasa ya kulitekeleza hilo jambo. Kukosekana kwa hamasa kutapelekea kulihairisha hilo j… Read More
  • Uwekaji Mipango UsioaminikaNi asili yetu kuwa na matumaini mema juu ya jambo fulani ambayo yamepitiliza uhalisia. Mfano tunadhani kuwa tutafanya mambo mengi kwa muda mchache kuliko inavyotakiwa kiuhalisia au kudhani jambo unalolifanya litachukua muda m… Read More
  • Maliza Robo ya Kwanza 2015 Hivi Hatua 3 muhimu unazohitaji kuzichukua ili kuweza kutumia muda wako kwa ufanisi na kupata matokeo ya ndoto yako kwa haraka: 1. Have a Plan Kuwa na mpango wa kina unaoanisha nini unachotaka kufanya na mpango huu ni lazima uw… Read More
  • Usipobadilika, utamezwa na mabadilikoYanapotokea mabadiliko jifunze kukabiliana nayo (kuadapt) kwa haraka vinginevyo utakavochelewa zaidi kwa kutafakari nini cha kufanya na kulialia na hali halisi utatumia gharama kubwa kuyapokea na muda utakuwa umekwenda pia. … Read More

0 comments:

Post a Comment