Monday, 17 October 2016

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Kipindi cha Mazoezi ya Vitendo


Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Kwa wanafunzi ambao wanasomea fani maalum katika elimu ya juu huwa mtaala wao unagawanywa katika vipindi viwili. Kipindi cha kwanza katika muhula huwa ni kujifunza kwa nadharia. Hapa wanafunzi hujifunza nadharia mbalimbali kuhusiana na mambo yanayohusu fani waliyoichagua. Kipindi cha pili katika muhula huwa ni kujifunza kwa vitendo. Hapa wanafunzi huwekwa katika mazingira halisi ya kazi na kuanza kuelekezwa hatua kwa hatua jinsi ya kutumia maarifa aliyoyapata darasani katika kuzalisha matokeo.

Ni mara chache utakuta chuo ulipotoka wamekupa mwongozo wa mambo gani hasa unatakiwa kuyafanya kwa kipindi unaenda mazoezi ya vitendo. Kitendea kazi ambacho chuo watakupa ni logbook, hapa utajaza mambo ambayo umeyafanya kwa kipindi chote cha mazoezi ya vitendo.

Vilevile kwa upande wa kampuni ambayo unaenda kufanya mazoezi ya vitendo wanategemea utakuwa upo katika ngazi fulani nzuri ya kuweza kuzalisha matokeo chanya. Hapa wanakutazama kama mwajiriwa mwenzao. Kwa hiyo kuna wakati utakuta unaaagizwa kazi nyingine ambazo hufahamu namna ya kuzifanya, au ni mpya kabisa hujawahi kukutana nazo kabisa.

Rafiki ni muhimu utambue na kujiuliza maswali haya nani hasa ni mhusika mkuu katika kufanikisha mazoezi haya? Je, ni chuo ambako umetoka? Je, ni kampuni ambayo umeenda kufanya mazoezi? Katika maswali haya yote mhusika mkuu ni wewe ambaye ni mwanafunzi, chuo na kampuni ni wahusika washiriki tu ambao wanakusaidia kukamilisha jukumu lako.

Rafiki nimekutana na wanafunzi mbalimbali ambao nimekuwa nawasimamia katika mazoezi yao ya vitendo. Hapa ninapenda kukushirikisha mambo ambayo ukiyazingatia yatakusaidia kufaidika kipindi cha mazoezi na hata baada ya mazoezi.

(a) Weka Malengo
Ni vizuri ukaandika malengo ambayo unakusudia kuyafikia baada ya mazoezi ya vitendo. Kila siku asubuhi kabla hujaenda katika mazoezi andika mambo angalau kwa uchache matatu utakayoyafanya yatakayochangia kukufikisha katika malengo uliyojiwekea katika kipindi hiki. Inapofika jioni fanya tathmini ni kwa kiasi gani hatua ulizozichukua tangu siku ilipoanza zinachangia au zinaathiri kufikia malengo uliyojiwekea. Kama kuna mapungufu yaliyojitokeza hakikisha unaanza nayo kuyafanyia kazi katika siku inayofuata.

SOMA : Zingatia Haya Ili Uifanye Siku Yako Bora

(b) Tembea na Notibuku
Msimamizi wako wa mazoezi ya vitendo atakuelekeza mambo mengi mapya ambayo huenda hujakutana nayo katika mazingira ya chuo. Mmoja wa wanamafanikio maarufu Jim Rohn alisema katika moja ya semina alizokuwa anafanya kuwa usiamini uwezo wa akili yako katika kukumbuka unayofundishwa ila uwe mwanafunzi mzuri kwa kuyaandika yale unayofundishwa ili uweze kutumia wakati ujao. Kufanya hivi kunachangia kupeleka ujumbe kwa wanaokuzunguka ni jinsi gani uko makini na kiwango chako cha kuzingatia mafunzo unayoyapata katika kampuni husika.

(c) Tumia Intaneti Kuongeza Ufanisi
Matumizi ya mitandao ya kijamii yameteka sehemu kubwa ya jamii. Kamwe usijisahau muda wa kazi ukautumia kutembelea mitandao ya kijamii. Badala yake tumia intaneti hasa google kujifunza namna ya kuboresha jinsi ya kufanya kazi zinazoendana na mazingira uliyopo. Hakikisha unafanya kitu bora kupita matarajio yao lakini pia kiwe kinaacha alama kuwa ulifanya kitu kikawasaidia kuboresha ufanisi katika kazi zao za kila siku. Hakikisha kipindi unamaliza mazoezi ya vitendo unawaacha katika hali bora kuliko kipindi umejiunga kufanya mazoezi.

SOMA : Umakini Unaouhitaji Kabla Hujaanza Kufanya Lolote

Rafiki mambo mengine ya kuzingatia ni kuhakikisha unakuwa nadhifu katika mavazi na kazi unazofanya, kufika kwa wakati katika eneo la mazoezi ya vitendo, kutoa taarifa kwa msimamizi endapo hautaweza kuhudhuria kutokana na dharula yoyote, kuuliza maswali mengi kadiri unavyoweza, kuwa tayari kufanya kazi za ziada ili kujifunza zaidi, na kadhalika.

Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Related Posts:

  • Maliza Robo ya Kwanza 2015 Hivi Hatua 3 muhimu unazohitaji kuzichukua ili kuweza kutumia muda wako kwa ufanisi na kupata matokeo ya ndoto yako kwa haraka: 1. Have a Plan Kuwa na mpango wa kina unaoanisha nini unachotaka kufanya na mpango huu ni lazima uw… Read More
  • Njia Rahisi Kuzuia Utendaji MbovuKama hali yetu ya hamasa ya kufanya jambo fulani haifanani/haiendani na jambo tunalohitajika kulifanya, moja kwa moja inapelekea kukosa hamasa ya kulitekeleza hilo jambo. Kukosekana kwa hamasa kutapelekea kulihairisha hilo j… Read More
  • Umakini Unaouhitaji Kabla Hujaanza Kufanya LoloteKutegemeana mtu na mtu kuna tofauti kati ya vitu vinavyoleta bugudha wakati unafanya jambo. Mfano kuna mtu hawezi kufanya kazi katika mazingira yenye kelele au wakati redio inazungumza wakati huo huo kuna mwingine anaweza kuf… Read More
  • Usipobadilika, utamezwa na mabadilikoYanapotokea mabadiliko jifunze kukabiliana nayo (kuadapt) kwa haraka vinginevyo utakavochelewa zaidi kwa kutafakari nini cha kufanya na kulialia na hali halisi utatumia gharama kubwa kuyapokea na muda utakuwa umekwenda pia. … Read More
  • Uwekaji Mipango UsioaminikaNi asili yetu kuwa na matumaini mema juu ya jambo fulani ambayo yamepitiliza uhalisia. Mfano tunadhani kuwa tutafanya mambo mengi kwa muda mchache kuliko inavyotakiwa kiuhalisia au kudhani jambo unalolifanya litachukua muda m… Read More

0 comments:

Post a Comment