Friday, 7 October 2016

Unawezaje Kutofautisha TABLET na iPAD?

Habari rafiki,
Kutokana na maendeleo makubwa yanayotokea katika teknologia kumekuwa na vifaa vya aina mbalimbali vinatengenezwa ili kusaidia kwanza  kuendana na kasi ya ukuaji katika teknologia lakini pili kurahisha utaratibu wa kawaida wa utendaji kazi kwa kutumia vifaa hivi.
Ni hakika katika jamii yetu utakuwa umekutana na aina za simu ambazo zinakuwa na kioo kikubwa chenye saizi kuanzia inchi saba, nane au zaidi.Aidha kutegemeana na namna mtu husika anavyofahamu ama urahisi wa kutamka kutoka kwa mhusika inachangia sana katika kifaa husika kitakavyoitwa. Aina hizi za simu kitaalamu zinaitwa "Tablet".


Kuna makampuni ya aina mbalimbali ambayo wanatengeneza hizi "tablet". Kwa kuyaorodhesha ni Apple, Nokia,HP, Dell, Lenovo, Toshiba, Asus, Samsung, Google Nexus na kadhalika.
Katika hizi "tablet" kuna programu maalum ambayo inawekwa na mtengenezaji ili kumsaidia mtumiaji kutumia kifaa hiki. Programu hii
inatambulika kwa lugha ya kiingereza "Operating System". Kuna aina tatu maarufu za "Operating System" ambazo zinatumika katika "tablet";
1. Apple iOS
Hii ni "Operating System" ambayo imetengenezwa na kampuni ya Apple. Mara nyingi huwekwa katika bidhaa za kampuni hii tuu.
2. Google Android OS
Hii ni "Operating System" ambayo imetengenezwa na kampuni ya Google. Hizi hutumiwa na kampuni zingine pia sio Google peke yake lakini hazitumiwi na kampuni ya Apple.
3. Microsoft Windows Phone OS
Hii ni "Operating System" ambayo imetengenezwa na kampuni ya Microsoft. Hizi hutumiwa mara nyingi na bidhaa za kampuni ya Nokia.
"Tablet" ambazo zimetengenezwa na kampuni ya Apple zinatumia "operating system" ya iOS. Hizi zinafahamika kwa jina maarufu la "iPad". Ni jina ambalo kampuni ya Apple wanatumia kuzitambulisha "tablet" zao kwa wateja.
"Tablet" zingine ambazo zimetengenezwa na kampuni nyingine kama nilivyoorodhesha hapo juu hutumia "operating system" aidha ya Android au Windows. Hizi ndiyo ambazo hutumia jina la "tablet".
Kwa mfano kama unatumia "tablet" iliyotengenezwa na kampuni ya Samsung si sahihi kuiita iPad bali unapaswa kuiita "tablet" au "Samsung Tablet".
N.B:
Aina nyingine za "operating system" zinazotumika katika simu ni Symbian OS, web OS, Blackberry OS na kadhalika.
Endelea kutembelea blogu hii kujifunza zaidi.

Related Posts:

  • Usipobadilika, utamezwa na mabadilikoYanapotokea mabadiliko jifunze kukabiliana nayo (kuadapt) kwa haraka vinginevyo utakavochelewa zaidi kwa kutafakari nini cha kufanya na kulialia na hali halisi utatumia gharama kubwa kuyapokea na muda utakuwa umekwenda pia. … Read More
  • Umakini Unaouhitaji Kabla Hujaanza Kufanya LoloteKutegemeana mtu na mtu kuna tofauti kati ya vitu vinavyoleta bugudha wakati unafanya jambo. Mfano kuna mtu hawezi kufanya kazi katika mazingira yenye kelele au wakati redio inazungumza wakati huo huo kuna mwingine anaweza kuf… Read More
  • Njia Rahisi Kuzuia Utendaji MbovuKama hali yetu ya hamasa ya kufanya jambo fulani haifanani/haiendani na jambo tunalohitajika kulifanya, moja kwa moja inapelekea kukosa hamasa ya kulitekeleza hilo jambo. Kukosekana kwa hamasa kutapelekea kulihairisha hilo j… Read More
  • Uwekaji Mipango UsioaminikaNi asili yetu kuwa na matumaini mema juu ya jambo fulani ambayo yamepitiliza uhalisia. Mfano tunadhani kuwa tutafanya mambo mengi kwa muda mchache kuliko inavyotakiwa kiuhalisia au kudhani jambo unalolifanya litachukua muda m… Read More
  • Maliza Robo ya Kwanza 2015 Hivi Hatua 3 muhimu unazohitaji kuzichukua ili kuweza kutumia muda wako kwa ufanisi na kupata matokeo ya ndoto yako kwa haraka: 1. Have a Plan Kuwa na mpango wa kina unaoanisha nini unachotaka kufanya na mpango huu ni lazima uw… Read More

2 comments:

  1. Rafiki unajitahidi na umesonga mbele sana,mm bado saana,hebu tembelea www.umburifodders.blogspot.com then Ucoment

    ReplyDelete
    Replies
    1. Rafiki yangu Ludovick Anael, ahsante kwa kutembelea blogu hii. Nitafanya hivyo rafiki.

      Delete