Sunday 15 March 2015

Je, Umepoteza Ujasiri (Confidence)?

Katika jambo lolote unalofanya unahitaji kuwa na ujasiri ili uweze kuwa na nguvu au stamina ya kuweza kulileta katika uhasilia(kulikamilisha) bila kujali vikwazo utakavyokutana navyo njiani.

Zifuatazo ni njia au namna ambavyo unaweza kuujenga ujasiri:

1. Shauku (passion) uliyonayo kulitekeleza jambo husika

2. Fahamu mambo ambayo una uwezo wa kufanya vizuri (strength zone) na uyafanye hayo kwa sababu tu ndiyo mambo ambayo utayafanya vizuri na Acha kufanya mambo usiyo na uwezo wa kuyafanya vizuri (weakness zone) kwa sababu hutayafanya vizuri na hauturuhusu mifumo iliyopo ikusaidie katika hayo maeneo usiyoyaweza

3. Fahamu lengo la wewe kuishi au kusudi ambalo Mungu anataka ulitimize (purpose of life) kwa wewe kuwepo hapa ulimwenguni

4. Unahitaji kuwa na utii (obedience)  kutimiza lile kusudi ambalo Mungu anataka ulitimize kwa wewe kuwepo hapa ulimwenguni

Kwa kifupi ujasiri unazalishwa hivi:

Shauku + Ushupavu + Kusudi + Utii = Ujasiri

au

Passion + Strength + Purpose + Obedience = Confidence

0 comments:

Post a Comment