Sunday 15 March 2015

Kanuni Inayoamua Wewe Kufanikiwa au Kushindwa

Katika mambo tunayofanya kuna matokeo mawili; aidha kufanikiwa sawasawa na malengo tuliyojiwekea kabla hatujanza kutekeleza jambo au kutokufanikiwa ambapo tunaweza kukuita kushindwa kutokana na kutofikia vigezo tulivyoviweka kuashiria kuwa jambo tumelifanikisha.

Kushindwa (failure) ni makosa madogo madogo katika maamuzi tunayorudia kuyafanya kila siku kuhusiana na jambo husika
(few error in judgment repeated everyday)

Wakati kufanikiwa (success) ni nidhamu au taaluma chache ambazo tunaziweka katika matendo kila siku kuhusiana na jambo husika
(few disciplines practiced everyday)

Kwa hivyo ulimbikizaji wa haya mambo madogo madogo kwa muda mrefu ndiyo hutupelekea kushindwa au kufanikiwa. Usidharau jambo dogo unalolifanya lichunguze kama hilo jambo unalolifanya ukilifanya kwa staili hiyo hiyo kwa muda mrefu litakuweka upande gani wa kushindwa au kufanikiwa? Kisha chukua hatua.

0 comments:

Post a Comment