Tuesday 17 March 2015

Tazama Kushindwa kwa Jicho Hili

Kushindwa hakuamaanishi wewe ndiye uliyeshindwa bali kunamaanisha hujafanikiwa bado

Kushindwa hakumaanishi haukutimiza/haujafanikisha kitu bali kunamaanisha umejifunza kitu

Kushindwa hakumaanishi wewe ni mjinga bali kunamaanisha unayo imani ya kutosha

Kushindwa hakumaanishi umeabika bali kunamaanisha una nia ya kujaribu

Kushindwa hakumaanishi hauna mbinu za kufanya kitu bali kunamaanisha unahitaji kufanya kwa mbinu tofauti

Kushindwa hakumaanishi umepoteza maisha bali kunamaanisha unayo sababu ya kuanza tena

Kushindwa hakumaanishi ukate tamaa bali kunamaanisha kujaribu tena kwa jitihada zaidi

Kushindwa hakumaanishi hautakamilisha bali kunamaanisha jambo unalofanya litachikua muda mrefu

Kushindwa hakumaanishi Mungu amekuacha bali kunamaanisha Mungu ana mawazo mazuri zaidi kwa ajili yako

Hauhitaji kuhofia kushindwa unaweza kuwa mtu unayetaka kuwa

No need to fear failure you can always become a person you want to be

0 comments:

Post a Comment