Saturday 14 March 2015

Namna Bora ya Kugawa Mapato Yako

Wakati unapopokea mapato/mshahara wako ugawe katika makundi haya 5 :



a) Sadaka
Kundi hili la fedha utalitumia kwa kufuata imani yako. Mara nyingi huwa ni asilimia kumi ya mapato.

b) Matumizi
Kundi hili la fedha ni kwa ajili ya kukuhudumia mahitaji yako ya kila siku. Huu huweza kuhusisha chakula, nauli kwa ajili ya kwenda sehemu unapofanya biashara/kazi n.k

c) Msaada
Kundi hili la fedha ni kwa ajili ya kutuma fedha kwa wale ndugu wanaokutegemea ili waweze kupata mahitaji yao ya kila siku. Mfano wazazi ambao wanakuwa hawawezi tena kufanya kazi kutokana na umri au kuumwa.

d) Dharura
Kundi hili la fedha ni kwa ajili ya kushughulika na misiba, ugonjwa na majanga ambayo yanaweza kukupata au kupata wanaokutegemea. Haya ni mambo yanayotokea kwa ghafla bila ya kuyatarajia

e) Kustaafu
Kundi hili la fedha ni kundi ambalo utalitumia kufanya uwekezaji, kuwekeza katika soko la hisa. Kundi hili halitakiwi kuguswa kabisa kwani ndilo linalotengeneza mfumo wa kukusaidia kipindi ambacho utakuwa huwezi kuzalisha/kufanya kazi

Kumbuka kadiri fedha yako inavyokua (financial growth) unahitaji pia kukuza misuli yako namna ya kuweza kuhimili/kudhibiti kiwango kikubwa cha fedha kwa kupata elimu endelevu ya fedha (financial education)

0 comments:

Post a Comment