Monday 16 March 2015

Mbinu za Kustahimili Matatizo

Siri moja kubwa ambayo imewafanya watu waliofanikiwa kuendelea vizuri ni mtazamo juu ya matatizo wanayokutana nayo. Ukizielewa kanuni hizi 6 kuhusu matatizo na kuzifanyia kazi ipasavyo wewe pia utakuwa mshindi.

1. Kila mtu anayo matatizo
(Every living human being has problems)
Usifikiri ukishafanikiwa utakuwa ndio umeyaaga matatizo, kadiri unavyofanikiwa ndivyo matatizo unayatengeneza mapya.
Inawezekana unafikiri ukipata kazi fulani ndo utakuwa umefanikiwa Sana, lakini kumbe unaweza kupata hiyo kazi lakini bosi wako akawa ni mkorofi. Sawa suluhisho unaweza kufikiri ni kujiajiri hapo pia utakutana na matatizo ya kushughulika na wafanyakazi wako ili wazalishe zaidi.
Kubaliana na uhalisia kuwa Hakuna mtu ambaye yuko huru hana matatizo


2. Kila tatizo lina ukomo wake
(Every problem has a limited life span)
Hakuna tatizo ambalo ni la kudumu yaani litakuwepo milele. Muda wa uhai wa tatizo ukiisha litakufa kwa kuisha/kutokuwepo kabisa.


3. Kila tatizo lina fursa
(Every problem holds positive possibilities)
Tatizo linaweza kuwa tatizo kwa mtu mmoja ila kwa mtu mwingine linaweza kuwa fursa. Hospitali zipo kwa sababu watu wanaumwa au wanasheria wapo kwa sababu kuna matatizo ya kisheria


4. Kila tatizo litakubadilisha
(Every problem will change you)
Hakuna tatizo ambalo litakuja katika maisha yetu na kutuacha kama lilivyotukuta. Tatizo litakufanya uamke au uchangamke na usonge mbele


5. Unao uwezo wa kuchagua tatizo likuathiri vipi/kwa kiwango gani
(You can choose what your problem will do to you)
Namna ambavyo unavyorespond tatizo linavyokutokea inaamua pia athari ya tatizo husika kwako.Inawezekana usiwe na uwezo wa kuchagua tatizo linalokutokea lakini unao uwezo wa kuchagua namna unavyorespond


6. Kuna namna chanya na hasi jinsi ya kurespond kwa kila tatizo
(There is a positive and negative reaction to every problem)
Mara zote chagua namna chanya ya kutatua tatizo kuliko namna hasi ya utatuzi wa tatizo. Jambo la msingi ni kuwa kama huwezi kutatua tatizo basi lisimamie kwa ubunifu


When you can't solve the problem, manage it creatively and constructively

0 comments:

Post a Comment