Monday 16 March 2015

Sumu ya Mafanikio

Unapokosa lengo kubwa katika maisha yako kwa kutokujua nini hasa unahitaji na unakipataje, mara nyingi hupelekea kutegemea maoni au ushauri wa watu wengine zaidi katika kuamua kitu cha kufanya kwa ajili ya maisha yako badala ya kujenga msingi katika kutafuta taarifa za kweli zilizo sahihi.

Kwa kutokuwa na taarifa za kweli zilizo sahihi itakupelekea kuahirisha jambo kwa kusema unasubiri mambo yawe mazuri ndiyo uanze kufanya kitu kwa ajili ya maisha yako.

Chukua hatua sasa na anza hapo ulipo kwa kutumia taarifa hizo hizo chache za kweli zilizo sahihi na rasilimali ulizonazo ufanye jambo kwa ajili ya maisha yako na baadae kadiri unavyoendelea utapata njia bora iliyo na ufanisi wa kuleta matokeo mazuri zaidi.

0 comments:

Post a Comment