Saturday, 14 March 2015

Fahamu Haya Kama Kiongozi

Kwa kila unayemuongoza unahusiana naye kwa kulingana na mojawapo kati ya ngazi hizi tano. Ngazi ya chini kabisa ni ngazi ya kwanza na ngazi ya juu kabisa ni ngazi ya tano:

1. Ngazi ya kwanza ambayo tunaanza nayo katika safari ya uongozi ni kupewa nafasi ya kuongoza (leadership position).
Katika nafasi hii watu walio chini yako wanakufuata kwa sababu ya nafasi yako hawaendi zaidi ya uwezo walionao na muda walio nao.

2. Ngazi ya pili inajengwa katika misingi ya mahusiano (relationship) na wale unaowaongoza. Watu unaowaongoza wanakufuata sio kwa sababu ya nafasi yako ya uongozi kama ngazi ya kwanza bali kwa sababu wanapenda namna unavyohusiana nao katika kuwaongoza. Hapa unakuwa umewapa nafasi ya kukusikiliza, kuona unachofanya na kujifunza.

3. Ngazi ya tatu inajengwa katika misingi ya uzalishaji/ufanisi.
Unaowaongoza watu kwa kuwa mfano katika uzalishaji na ufanisi katika mambo unayoyafanya. Hii itawasaidia kufanya kile wanachokiona na hivyo utakuwa umewavutia kuzalisha na kuweka mkazo katika ufanisi. Hapa ndipo matatizo mengi katika sehemu unayoongoza yanaweza kushughulikiwa.

4. Ngazi ya nne inajengwa katika misingi ya kuwaendeleza wale unaowaongoza ili kuongeza uwezo wao wa ufanisi/uzalishaji (developing people). Na hii itachangiwa kwa kuchagua watu sahihi na kuwaweka sehemu sahihi ambazo zinaendena na uwezo wao

5. Ngazi ya tano inajengwa katika misingi ya heshima. Umefanya mengi yanayowagusa wale unaowaongoza na hivyo kusababisha wakufuate. Wanakufuata kwa sababu ya mambo mengi uliyoyafanya kwa ubora kwa muda mrefu. Hii ni ngazi ya juu kabisa katika uongozi

Related Posts:

  • Je, Unajua?Ni bora kufanya kitu kisicho kamili kuliko kutokufanya chochote kisicho na dosari Better to do something imperfectly than to do nothing flawlessly… Read More
  • Fanya Haya ili Ukue1. Usitamani mambo yangekuwa marahisi, tamani ungekuwa bora mno Don't wish it were easier; wish you were better 2. Usitamani ungekutana au ungekuwa na matatizo machache,tamani ungekuwa na ujuzi zaidi Don't wish for less prob… Read More
  • Tazama Kushindwa kwa Jicho HiliKushindwa hakuamaanishi wewe ndiye uliyeshindwa bali kunamaanisha hujafanikiwa bado Kushindwa hakumaanishi haukutimiza/haujafanikisha kitu bali kunamaanisha umejifunza kitu Kushindwa hakumaanishi wewe ni mjinga bali kunamaa… Read More
  • Sumu ya MafanikioUnapokosa lengo kubwa katika maisha yako kwa kutokujua nini hasa unahitaji na unakipataje, mara nyingi hupelekea kutegemea maoni au ushauri wa watu wengine zaidi katika kuamua kitu cha kufanya kwa ajili ya maisha yako badala … Read More
  • Usipuuze TatizoMatatizo mengi kamwe hayatatuliwi au hayadhibiti kwa ufanisi kutokana na kutoyapa uzito wa kutosheleza. Hakuna tatizo ambalo halina umuhimu kiasi kuwa hatuhitaji kujali kuhusu hilo tatizo. Mfano kwa mwanafunzi inawezekena hap… Read More

0 comments:

Post a Comment