Kwa kila unayemuongoza unahusiana naye kwa kulingana na mojawapo kati ya ngazi hizi tano. Ngazi ya chini kabisa ni ngazi ya kwanza na ngazi ya juu kabisa ni ngazi ya tano:
1. Ngazi ya kwanza ambayo tunaanza nayo katika safari ya uongozi ni kupewa nafasi ya kuongoza (leadership position).
Katika nafasi hii watu walio chini yako wanakufuata kwa sababu ya nafasi yako hawaendi zaidi ya uwezo walionao na muda walio nao.
2. Ngazi ya pili inajengwa katika misingi ya mahusiano (relationship) na wale unaowaongoza. Watu unaowaongoza wanakufuata sio kwa sababu ya nafasi yako ya uongozi kama ngazi ya kwanza bali kwa sababu wanapenda namna unavyohusiana nao katika kuwaongoza. Hapa unakuwa umewapa nafasi ya kukusikiliza, kuona unachofanya na kujifunza.
3. Ngazi ya tatu inajengwa katika misingi ya uzalishaji/ufanisi.
Unaowaongoza watu kwa kuwa mfano katika uzalishaji na ufanisi katika mambo unayoyafanya. Hii itawasaidia kufanya kile wanachokiona na hivyo utakuwa umewavutia kuzalisha na kuweka mkazo katika ufanisi. Hapa ndipo matatizo mengi katika sehemu unayoongoza yanaweza kushughulikiwa.
4. Ngazi ya nne inajengwa katika misingi ya kuwaendeleza wale unaowaongoza ili kuongeza uwezo wao wa ufanisi/uzalishaji (developing people). Na hii itachangiwa kwa kuchagua watu sahihi na kuwaweka sehemu sahihi ambazo zinaendena na uwezo wao
5. Ngazi ya tano inajengwa katika misingi ya heshima. Umefanya mengi yanayowagusa wale unaowaongoza na hivyo kusababisha wakufuate. Wanakufuata kwa sababu ya mambo mengi uliyoyafanya kwa ubora kwa muda mrefu. Hii ni ngazi ya juu kabisa katika uongozi
Fahamu Haya Kama Kiongozi
Related Posts:
Unahitaji Wastani wa Maswali 12 KufanikiwaUnapofanya maamuzi ya kutaka kufanikiwa unahitaji kufanya mabadiliko ya msingi (fundamental change).Ili kufanya mabadiliko unahitaji namna nzuri ya kuelewa sehemu ambayo unatakiwa kuanzia. Sehemu iliyo bora kabisa ya kuanza… Read More
Fahamu Haya Kama KiongoziKwa kila unayemuongoza unahusiana naye kwa kulingana na mojawapo kati ya ngazi hizi tano. Ngazi ya chini kabisa ni ngazi ya kwanza na ngazi ya juu kabisa ni ngazi ya tano: 1. Ngazi ya kwanza ambayo tunaanza nayo katika safar… Read More
Mbinu za Kustahimili MatatizoSiri moja kubwa ambayo imewafanya watu waliofanikiwa kuendelea vizuri ni mtazamo juu ya matatizo wanayokutana nayo. Ukizielewa kanuni hizi 6 kuhusu matatizo na kuzifanyia kazi ipasavyo wewe pia utakuwa mshindi. 1. Kila mtu a… Read More
Je, Umepoteza Ujasiri (Confidence)?Katika jambo lolote unalofanya unahitaji kuwa na ujasiri ili uweze kuwa na nguvu au stamina ya kuweza kulileta katika uhasilia(kulikamilisha) bila kujali vikwazo utakavyokutana navyo njiani. Zifuatazo ni njia au namna ambavy… Read More
Kanuni Inayoamua Wewe Kufanikiwa au KushindwaKatika mambo tunayofanya kuna matokeo mawili; aidha kufanikiwa sawasawa na malengo tuliyojiwekea kabla hatujanza kutekeleza jambo au kutokufanikiwa ambapo tunaweza kukuita kushindwa kutokana na kutofikia vigezo tulivyoviweka … Read More
0 comments:
Post a Comment