Monday, 16 March 2015

Mbinu za Kustahimili Matatizo

Siri moja kubwa ambayo imewafanya watu waliofanikiwa kuendelea vizuri ni mtazamo juu ya matatizo wanayokutana nayo. Ukizielewa kanuni hizi 6 kuhusu matatizo na kuzifanyia kazi ipasavyo wewe pia utakuwa mshindi.

1. Kila mtu anayo matatizo
(Every living human being has problems)
Usifikiri ukishafanikiwa utakuwa ndio umeyaaga matatizo, kadiri unavyofanikiwa ndivyo matatizo unayatengeneza mapya.
Inawezekana unafikiri ukipata kazi fulani ndo utakuwa umefanikiwa Sana, lakini kumbe unaweza kupata hiyo kazi lakini bosi wako akawa ni mkorofi. Sawa suluhisho unaweza kufikiri ni kujiajiri hapo pia utakutana na matatizo ya kushughulika na wafanyakazi wako ili wazalishe zaidi.
Kubaliana na uhalisia kuwa Hakuna mtu ambaye yuko huru hana matatizo


2. Kila tatizo lina ukomo wake
(Every problem has a limited life span)
Hakuna tatizo ambalo ni la kudumu yaani litakuwepo milele. Muda wa uhai wa tatizo ukiisha litakufa kwa kuisha/kutokuwepo kabisa.


3. Kila tatizo lina fursa
(Every problem holds positive possibilities)
Tatizo linaweza kuwa tatizo kwa mtu mmoja ila kwa mtu mwingine linaweza kuwa fursa. Hospitali zipo kwa sababu watu wanaumwa au wanasheria wapo kwa sababu kuna matatizo ya kisheria


4. Kila tatizo litakubadilisha
(Every problem will change you)
Hakuna tatizo ambalo litakuja katika maisha yetu na kutuacha kama lilivyotukuta. Tatizo litakufanya uamke au uchangamke na usonge mbele


5. Unao uwezo wa kuchagua tatizo likuathiri vipi/kwa kiwango gani
(You can choose what your problem will do to you)
Namna ambavyo unavyorespond tatizo linavyokutokea inaamua pia athari ya tatizo husika kwako.Inawezekana usiwe na uwezo wa kuchagua tatizo linalokutokea lakini unao uwezo wa kuchagua namna unavyorespond


6. Kuna namna chanya na hasi jinsi ya kurespond kwa kila tatizo
(There is a positive and negative reaction to every problem)
Mara zote chagua namna chanya ya kutatua tatizo kuliko namna hasi ya utatuzi wa tatizo. Jambo la msingi ni kuwa kama huwezi kutatua tatizo basi lisimamie kwa ubunifu


When you can't solve the problem, manage it creatively and constructively

Related Posts:

  • Je, Umepoteza Ujasiri (Confidence)?Katika jambo lolote unalofanya unahitaji kuwa na ujasiri ili uweze kuwa na nguvu au stamina ya kuweza kulileta katika uhasilia(kulikamilisha) bila kujali vikwazo utakavyokutana navyo njiani. Zifuatazo ni njia au namna ambavy… Read More
  • Unahitaji Wastani wa Maswali 12 KufanikiwaUnapofanya maamuzi ya kutaka kufanikiwa unahitaji kufanya mabadiliko ya msingi (fundamental change).Ili kufanya mabadiliko unahitaji namna nzuri ya kuelewa sehemu ambayo unatakiwa kuanzia. Sehemu iliyo bora kabisa ya kuanza… Read More
  • Fahamu Haya Kama KiongoziKwa kila unayemuongoza unahusiana naye kwa kulingana na mojawapo kati ya ngazi hizi tano. Ngazi ya chini kabisa ni ngazi ya kwanza na ngazi ya juu kabisa ni ngazi ya tano: 1. Ngazi ya kwanza ambayo tunaanza nayo katika safar… Read More
  • Jenga Mtazamo Huu Unapouliza MaswaliTukio lolote linapotutokea bila kujali ni zuri au baya katika akili kuna mambo matatu huwa yanaendelea: a) Fikra (thoughts) b) Hisia (feelings) c) Hali (circumstances) Bila kujali hali ya tukio mambo hayo 3 ndiyo yanayotuon… Read More
  • Kanuni Inayoamua Wewe Kufanikiwa au KushindwaKatika mambo tunayofanya kuna matokeo mawili; aidha kufanikiwa sawasawa na malengo tuliyojiwekea kabla hatujanza kutekeleza jambo au kutokufanikiwa ambapo tunaweza kukuita kushindwa kutokana na kutofikia vigezo tulivyoviweka … Read More

0 comments:

Post a Comment