Saturday, 14 March 2015

Jenga Mtazamo Huu Unapouliza Maswali

Tukio lolote linapotutokea bila kujali ni zuri au baya katika akili kuna mambo matatu huwa yanaendelea:

a) Fikra (thoughts)
b) Hisia (feelings)
c) Hali (circumstances)

Bila kujali hali ya tukio mambo hayo 3 ndiyo yanayotuongoza kwa sehemu kubwa namna tutakavyochagua jinsi tutaitikia (kurespond) katika tukio husika.

Mara nyingi husahaulika kuwa hatua ya utekelezaji katika matendo hufuata baada ya hatua ya kuuliza maswali.

Kwa nini hatua ya kuuliza maswali itangulie kabla ya hatua ya utekelezaji katika matendo? Umuhimu wa kuuliza maswali upo katika:

a) Kukusanya taarifa za kina
b) Kujenga uelewa na kujifunza
c) Kujenga, kuboresha na kuendeleza mahusiano
d) Kufafanua na kuthibitisha ulichosikiliza/ulichokiona/ulichokipokea
e) Kuchochea ubunifu na uvumbuzi
f) Kujenga ushirikiano
g) Kuweka malengo na kutengeneza mpango kazi
h) Kuchunguza, kugundua na kutengeneza nafasi/fursa mpya

Hivyo maswali tunayojiuliza wenyewe hutupatia fursa kwa ajili ya kufikiri na kuwezekana kwa namna ya kipekee kwa jambo husika tofauti na vile kabla hatujajiuliza hayo maswali.
Na jinsi utakavyoweza kuuliza maswali kwa ufasaha/kina zaidi ndivyo utaweza pia kupata matokeo makubwa zaidi

Related Posts:

  • Je, Unafahamu Kifaa Kinachoitwa Mouse? Habari rafiki, Kompyuta huundwa na vifaa vilivyogawanyika katika makundi makuu matatu. Makundi haya yamewekwa kutegemeana na kazi zinazotekelezwa na vifaa vinavyoundwa kundi husika. 1. Kundi la kwanza linajumuisha vi… Read More
  • Jinsi ya Kufanya Partition Katika Hard DriveHabari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Partition katika kompyuta ni kitendo cha kugawa hard drive katika sehemu mbalimbali. Kitendo hiki husaidia kutenganisha sehemu ya ha… Read More
  • Hatua Nne (04) Katika Uandishi wa Blogu Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki unapoanza kuandika makala katika blogu kuna changamoto mbalimbali ambazo utakutana nazo. Changamoto hizi zinatokana na kuwa … Read More
  • Mfumo Pekee Utakakokusaidia Kukidhi Mahitaji ya Mteja Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Suala la kukidhi mahitaji ya mteja unaowahudumia linakwenda sambamba na utoaji wa huduma bora kwa mteja. Kiwango cha kukidhi mahita… Read More
  • Jinsi ya Kutatua Tatizo la Barua Pepe Kutoingia Katika InboxHabari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Barua pepe ni njia ambayo watumiaji wa kompyuta hutumia kutuma ujumbe kwa njia ya kidigitali. Kuna kampuni za aina mbalimbali ambazo… Read More

0 comments:

Post a Comment