Saturday, 14 March 2015

Jenga Mtazamo Huu Unapouliza Maswali

Tukio lolote linapotutokea bila kujali ni zuri au baya katika akili kuna mambo matatu huwa yanaendelea:

a) Fikra (thoughts)
b) Hisia (feelings)
c) Hali (circumstances)

Bila kujali hali ya tukio mambo hayo 3 ndiyo yanayotuongoza kwa sehemu kubwa namna tutakavyochagua jinsi tutaitikia (kurespond) katika tukio husika.

Mara nyingi husahaulika kuwa hatua ya utekelezaji katika matendo hufuata baada ya hatua ya kuuliza maswali.

Kwa nini hatua ya kuuliza maswali itangulie kabla ya hatua ya utekelezaji katika matendo? Umuhimu wa kuuliza maswali upo katika:

a) Kukusanya taarifa za kina
b) Kujenga uelewa na kujifunza
c) Kujenga, kuboresha na kuendeleza mahusiano
d) Kufafanua na kuthibitisha ulichosikiliza/ulichokiona/ulichokipokea
e) Kuchochea ubunifu na uvumbuzi
f) Kujenga ushirikiano
g) Kuweka malengo na kutengeneza mpango kazi
h) Kuchunguza, kugundua na kutengeneza nafasi/fursa mpya

Hivyo maswali tunayojiuliza wenyewe hutupatia fursa kwa ajili ya kufikiri na kuwezekana kwa namna ya kipekee kwa jambo husika tofauti na vile kabla hatujajiuliza hayo maswali.
Na jinsi utakavyoweza kuuliza maswali kwa ufasaha/kina zaidi ndivyo utaweza pia kupata matokeo makubwa zaidi

Related Posts:

  • Faida Tatu (03) za Biashara Inayoendeshwa Kwa Intaneti Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki katika zama za viwanda (industrial age) bidhaa nyingi zilizokuwa zinauzwa zipo physical kiasili. Bidhaa hizi mpaka uzinunue … Read More
  • Uchambuzi wa Kitabu cha " EAT THAT FROG"Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Brian Tracy ni mwandishi wa kitabu cha "EAT THAT FROG". Brian ni mwalimu mwenye uzoefu sana katika eneo la mafanikio. Mambo mengi amb… Read More
  • Jinsi Ya Kuishinda Hofu Uliyonayo Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki katika maisha watu wamekuwa wakitawaliwa na hofu, wameipa hofu nafasi kubwa ya kutawala maisha yao. Hofu huzaa malalamiko ku… Read More
  • Mambo Matano (05) Yanayosababisha KushindwaHabari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki si wote wanajifunza kutokana na makosa wanayoyafanya au kutambua mapema makosa waliyoyafanya ili wasiyarudie. Kuwa na mwongozo… Read More
  • Mambo Matano (05) Yaliyojificha Katika Mafanikio Yako Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki watu wengi wamekuwa wakipima mafanikio kwa kiwango cha vitu vinavyomilikiwa na mhusika. Kutokana na hili kunakuwa na maana m… Read More

0 comments:

Post a Comment