Tuesday, 11 October 2016

Maana za Vibao Vya Namba Za Magari (Plate Number)

Habari rafiki!
Katika kila gari kuna sehemu mbili ambapo huwekwa vibao vyenye namba kwa ajili ya kulitambulisha gari husika. Vibao hivi huwekwa mbele na nyuma ya gari. Katika lugha ya kiingereza huitwa "plate number". Katika makala ya leo ninakushirikisha namna ya kupata ujumbe unaowasilishwa na pindi unaposoma kibao husika cha namba ya gari.


Aina za Vibao vya Namba za Magari
1. Kibao chenye rangi ya njano na namba inayoanza na herufi T
Kibao hiki kinabeba maana kuwa gari husika limesajiliwa kutumika kwa ajili ya shughuli binafsi. Kwa kiingereza inasemwa "private use". Magari yenye vibao hivi hayaruhusiwi kutumika kwa ajili ya biashara.
2. Kibao chenye rangi nyeupe na namba inayoanza na herufi T
Kibao hiki kinabeba maana kuwa gari husika limesajiliwa kwa ajili ya matumizi ya biashara. Kwa kiingereza inasemwa "commercial use". Mfano mzuri daladala au basi za kubeba abiria na taxi.
3. Kibao chenye rangi ya njano na namba haianzi na herufi T
Kibao hiki kinabeba maana kuwa gari husika linamilikiwa na taasisi ya umma au serikali. Hapa kuna makundi yafuatayo:
(a) SU - shirika la umma , mfano vyuo vikuu vya serikali
(b) SM - Serikali za Mitaa , mfano ni halmashauri
(c) STK,STL,STJ - serikali, mfano ni wizara
4. Kibao chenye rangi nyekundu na namba inayoanza na herufi DFP au DFPA
Kibao hiki kinabeba maana kuwa gari husika limetolewa kwa ajili ya matumizi ya miradi inayofadhiliwa na wafadhili kutoka nje ya nchi.
5. Kibao chenye rangi ya bluu na namba inayoanza na herufi T kufuatiwa na namba na kisha herufi CD
Kibao hiki kinabeba maana kuwa gari husika linamilikiwa na moja ya shirika la umoja wa mataifa. Mfano shirika la Afya Duniani (WHO).
6. Kibao chenye rangi ya kijani na namba inayoanza na herufi T kufuatiwa na namba na kisha herufi CD
Kibao hiki kinabeba maana kuwa gari husika linamilikiwa na ofisi za ubalozi wa nchi fulani. Mfano ubalozi wa Ufaransa.
7. Kibao chenye rangi nyeusi na namba zimeandiwa kwa rangi ya njano
Kibao hiki kinabeba maana kuwa gari husika linamilikiwa na Jeshi la  Polisi. Namba hizi huwa na herufi PT
8. Kibao chenye rangi nyeusi na namba zimeandiwa kwa rangi ya njano
Kibao hiki kinabeba maana kuwa gari husika linamilikiwa na Jeshi la Wananchi (JW). Namba hizi huwa na herufi JW.
9. Kibao chenye rangi ya kijani na namba zenye herufi MT
Kibao hiki kinabeba maana kuwa gari husika linamilikiwa na Jeshi la Magereza.
Unaweza kubofya hapa ili kuweka barua pepe yako au rafiki yako ambaye unapenda makala hizi azipate moja kwa moja katika barua pepe.

Related Posts:

  • Jinsi ya Kutumia Kompyuta Yako Kuwa Chanzo cha Intaneti Habari rafiki! Katika makala ya leo ninapenda kukushirikisha namna ya "kushare" intaneti kutoka kwenye kompyuta na kwenda kwenye vifaa vingine vyenye uwezo wa kupokea intaneti. Kompyuta yoyote ambayo ina kifaa kinachoitwa "… Read More
  • Utaratibu Sahihi wa Uandishi wa Saa Habari rafiki! Kumekuwa na changamoto katika kujua namna sahihi ya uandishi wa muda kutoka katika saa.Saa ni kifaa ambacho kinatumika kusoma muda ambao huwa katika mpangilio wa kuanza na saa, kisha kufuata dakika na kuishia… Read More
  • Uchambuzi wa Kitabu cha ONE MINUTE MANAGER Habari rafiki yangu ambaye unaendelea kufuatilia makala katika blogu hii, wiki hii nilifanikiwa kusoma kitabu kinachoitwa One Minute Manager, hapa chini nimekushirikisha mambo ambayo nilijifunza na kuyanote ili kuweza kutusa… Read More
  • Maana za Vibao Vya Namba Za Magari (Plate Number) Habari rafiki! Katika kila gari kuna sehemu mbili ambapo huwekwa vibao vyenye namba kwa ajili ya kulitambulisha gari husika. Vibao hivi huwekwa mbele na nyuma ya gari. Katika lugha ya kiingereza huitwa "plate number". Katik… Read More
  • Uandishi Sahihi wa Siku na Mwezi Katika Mwaka Habari rafiki mfuatiliaji wa makala mbalimbali katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Muda unaweza kuoneshwa kwa vipimo mbalimbali. Kipimo kidogo  cha muda ni sekunde. Sekunde zikikusanyika na kufika idadi ya siti… Read More

24 comments:

  1. Nzuriii hii nimeipenda..👏👏

    ReplyDelete
  2. Kuna ambazo zina kibao cha kijani namba zinaanza RAC halafu zinafuatia namba, hizo zina maana gani?

    ReplyDelete
  3. Kuna gari plate number yake ina nyota tatu (***)

    ReplyDelete
  4. Hii ni nzuri.... itapendeza pia tukijua kirefu cha STL, STK,STJ...

    ReplyDelete
  5. Vip huhusu kibao cha rangi nyeusi na namba zake rangi nyeupe na nyingine rangi ya njano na inaanza na J harafu namba na nyingine njano na inaanza heruf M harafu inafuatiwa na namba vip nayo imekaaje?

    ReplyDelete