Wednesday, 16 November 2016

Faida Tatu (03) za Biashara Inayoendeshwa Kwa Intaneti

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Rafiki katika zama za viwanda (industrial age) bidhaa nyingi zilizokuwa zinauzwa zipo physical kiasili. Bidhaa hizi mpaka uzinunue ulihitaji kuzishika au kuziona kwa kukutana na muuzaji ana kwa ana. Lakini leo hii tupo katika zama za habari (information age) ambapo mambo ni tofauti na kipindi cha nyuma.





Hapa ninakushirikisha faida utakazozipata kwa kuwa na biashara inayoendeshwa kwa kutumia teknologia ya intaneti.
Soma Makala Hii Inayohusiana : Mambo Matano (05) Yanayosababisha Kushindwa
(a) Uwepo Wako Katika Eneo la Biashara
Katika zama za viwanda biashara inakuhitaji kuwepo katika eneo la biashara muda wote ili kuiendesha (full time). Lakini biashara inayoendeshwa kwa teknologia ya intaneti unahitaji idadi ya masaa mawili au matatu kuiendesha hauhitaji kuwepo eneo la biashara muda wote (part time). Mfano wa biashara hii ni blogu ambapo muda utakaoutumia ni ule ambao unatengeneza makala.
(b)  Masoko
Katika zama za viwanda biashara inaendeshwa katika maeneo yale ambayo bidhaa yako inafika ,hivyo siku lako sio pana. Lakini katika zama za taarifa biashara inaendeshwa katika eneo pana zaidi,kwa sababu soko lako ni mtandaoni, hivyo kila mtu anayeweza kuingia mtandaoni anakuwa ni mmoja kati ya wale waliopo katika soko lako.
(c) Muda wa Kutoa Huduma
Katika zama za viwanda masaa ya kufanya kazi au biashara ni muda ule ambao watu wanakuwa eneo la biashara , huu muda unaitwa muda wa kazi (office hours). Lakini katika zama za taarifa masaa ya kufanya kazi ni masaa 24 kutokana na huduma kupatikana katika mtandao muda wote.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.
Goodluck Moshi
Author
StadizaMafanikio

Related Posts:

  • Umakini Unaouhitaji Kabla Hujaanza Kufanya LoloteKutegemeana mtu na mtu kuna tofauti kati ya vitu vinavyoleta bugudha wakati unafanya jambo. Mfano kuna mtu hawezi kufanya kazi katika mazingira yenye kelele au wakati redio inazungumza wakati huo huo kuna mwingine anaweza kuf… Read More
  • Njia Rahisi Kuzuia Utendaji MbovuKama hali yetu ya hamasa ya kufanya jambo fulani haifanani/haiendani na jambo tunalohitajika kulifanya, moja kwa moja inapelekea kukosa hamasa ya kulitekeleza hilo jambo. Kukosekana kwa hamasa kutapelekea kulihairisha hilo j… Read More
  • Jenga Mtazamo Huu Unapouliza MaswaliTukio lolote linapotutokea bila kujali ni zuri au baya katika akili kuna mambo matatu huwa yanaendelea: a) Fikra (thoughts) b) Hisia (feelings) c) Hali (circumstances) Bila kujali hali ya tukio mambo hayo 3 ndiyo yanayotuon… Read More
  • Maliza Robo ya Kwanza 2015 Hivi Hatua 3 muhimu unazohitaji kuzichukua ili kuweza kutumia muda wako kwa ufanisi na kupata matokeo ya ndoto yako kwa haraka: 1. Have a Plan Kuwa na mpango wa kina unaoanisha nini unachotaka kufanya na mpango huu ni lazima uw… Read More
  • Uwekaji Mipango UsioaminikaNi asili yetu kuwa na matumaini mema juu ya jambo fulani ambayo yamepitiliza uhalisia. Mfano tunadhani kuwa tutafanya mambo mengi kwa muda mchache kuliko inavyotakiwa kiuhalisia au kudhani jambo unalolifanya litachukua muda m… Read More

0 comments:

Post a Comment