Friday, 11 November 2016

Jinsi Ya Kuishinda Hofu Uliyonayo

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Rafiki katika maisha watu wamekuwa wakitawaliwa na hofu, wameipa hofu nafasi kubwa ya kutawala maisha yao. Hofu huzaa malalamiko kunakosababishwa na hali ya kutoridhika na hatua au hali uliyonayo. Lakini ukifanya ulinganisho kati ya vile ulivyonavyo na walivyonavyo wengine,utagundua unahitaji kuwa na moyo wa shukrani.



Utafiti unaonesha asilimia tisini ya mambo au vitu katika maisha yetu ni sahihi au sawa (right), wakati asilimia kumi ya mambo au vitu katika maisha ndiyo haviko sahihi (wrong). Ikiwa unataka kuwa na furaha hakikisha unaegemea zaidi katika upande wa mambo yaliyo sahihi (asilimia tisini) kuliko yasiyo sahihi (asilimia kumi). Na ikiwa unataka kuishi maisha ya masikitiko au huzuni hakikisha unachagua kuegemea zaidi katika upande wa mambo yasiyo sahihi (asilimia kumi) kuliko yaliyo sahihi (asilimia tisini).
Ni mara chache sana tunatumia wakati kufikiri yale ambayo tunayo, badala yake utakuta  tunawaza kuhusu yale ambayo hatuna. Usilalamike kama vile upo wewe peke yako ndiye mwenye matatizo au ambaye hana. Ukichunguza utagundua una mambo mengi sana ya kukufanya uwe na shukrani kutokana na kuwa na upekee hasa ukilinganisha na wengine ambao hawana vitu ulivyonavyo. Hapa rafiki ninapenda kukusisitiza kuamua kwa kukusudia kuangalia upande wa uzuri kuliko upande wa ubaya wa kila tukio linalokuja katika maisha yako.
Rafiki napenda kusisitiza usihesabu idadi ya matatizo uliyonayo anza kuhesabu mambo mazuri uliyonayo, hii itakusaidia kuondoa hofu ya kuishi.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.
Goodluck Moshi
Author
StadizaMafanikio

Related Posts:

  • Usipobadilika, utamezwa na mabadilikoYanapotokea mabadiliko jifunze kukabiliana nayo (kuadapt) kwa haraka vinginevyo utakavochelewa zaidi kwa kutafakari nini cha kufanya na kulialia na hali halisi utatumia gharama kubwa kuyapokea na muda utakuwa umekwenda pia. … Read More
  • Maliza Robo ya Kwanza 2015 Hivi Hatua 3 muhimu unazohitaji kuzichukua ili kuweza kutumia muda wako kwa ufanisi na kupata matokeo ya ndoto yako kwa haraka: 1. Have a Plan Kuwa na mpango wa kina unaoanisha nini unachotaka kufanya na mpango huu ni lazima uw… Read More
  • Msingi wa kutimiza maisha yenye ufanisiUwezo uliopo ndani yetu ni mkubwa sana kuliko kile ambacho tumeshakitendea haki kwa nafasi zetu tulizonazo kwa kutendea ulimwengu. Maswali haya yatakusaidia kutafakari kitu gani ambacho unacho ndani yako bado hujakileta ulimw… Read More
  • Uwekaji Mipango UsioaminikaNi asili yetu kuwa na matumaini mema juu ya jambo fulani ambayo yamepitiliza uhalisia. Mfano tunadhani kuwa tutafanya mambo mengi kwa muda mchache kuliko inavyotakiwa kiuhalisia au kudhani jambo unalolifanya litachukua muda m… Read More
  • Fursa nyingi, Muda mchache na Rasilimali chache, Nifanyaje?Ukifanya uchambuzi kwa kulinganisha kundi la "shughuli na fursa" na kundi la "muda na rasimali" utapata hitimisho ya kuona katika kundi la "shughuli na fursa" zipo nyingi kuliko kundi la "muda na rasilimali" tulizonazo kwa aj… Read More

0 comments:

Post a Comment