Tuesday, 15 November 2016

Mambo Matano (05) Yanayosababisha Kushindwa

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!

Rafiki si wote wanajifunza kutokana na makosa wanayoyafanya au kutambua mapema makosa waliyoyafanya ili wasiyarudie. Kuwa na mwongozo kutasaidia sana kujua namna ya kuenenda katika mambo haya.

Katika maisha ya kila siku kuna mambo matano yanayosababisha kushindwa. Ukiyafahamu na kujua jinsi ya kuyakabili utakuwa umesaidia kuondoa vizuizi katika njia yako ya kuelekea mafanikio.

Jambo la kwanza ni kulaumu wengine kuwa ndiyo wamesababisha kutokea kushindwa. Hii hali hujitokeza kipindi ambapo kosa limetokea badala ya kubeba wajibu wa kuuliza mambo gani yamechangia kuwafikisha katika kushindwa badala yake unamtafuta mtu wa kumlaumu kama yeye ndiye chanzo kikuu cha kushindwa.

Jambo la pili lipo kinyume na hilo la kwanza , hapa unakuta unajilaumu binafsi kuwa wewe ni chanzo cha kusababisha kushindwa. Hapa badala ya kupambana na tatizo lililosababisha kushindwa, kupambana ili kulitatua na kuzuia lisijirudie , badala yake unajilaumu. Suala kubwa si kushindwa je umeridhika na kushindwa huko, ukiridhika na kushindwa maana yake umekubaliana na hali na hujipatii nafasi ya kukua kupitia kujiendeleza binafsi.

Soma Makala Hii Inayohusiana : Namna ya Kutambua Dalili Za Kushindwa

Jambo la tatu ni kutokuwa na malengo. Kukosa malengo ni sawa na kutokuwa na uelekeo wa safari yako yaani unasafiri lakini hufahamu kituo cha mwisho cha safari yako. Kutokuwa na malengo kunasababisha kutokuwa na umakini wa kuzingatia wapi uweze kuelekeza nguvu na vipaji ambavyo umepewa na muumba wako.

Jambo la nne ni kutokuwa na malengo sahihi. Watu wengi wanafanya kosa la kutokupanga malengo yao wao wenyewe badala yake wanawaachia watu wengine kama wanafamilia au marafiki au mazingira kuwasaidia kupanga. Wanapofika mwisho wa safari ya kutimiza lengo husika wanakosa furaha kutokana na kukosa uhusiano wa lengo kutokuwa yeye ndiye mwanzilishi au umiliki wa lengo.

Jambo la tano ni kupenda kutumia short cut. Matumizi ya shortcut huonekana ni njia ya haraka ya kupata matokeo. Changamoto ya njia hii ni kuwa matokeo unayoyapata hayadumu yanakuwa ya muda mfupi , kwa sababu ili kupata matokeo ya kudumu ni lazima kazi ifanyike ambayo huhesabika kuwa ni gharama ya kufikia matokeo husika.

Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.

Goodluck Moshi
Author
StadizaMafanikio

Related Posts:

  • Mfumo Pekee Utakakokusaidia Kukidhi Mahitaji ya Mteja Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Suala la kukidhi mahitaji ya mteja unaowahudumia linakwenda sambamba na utoaji wa huduma bora kwa mteja. Kiwango cha kukidhi mahita… Read More
  • Jinsi ya Kufanya Partition Katika Hard DriveHabari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Partition katika kompyuta ni kitendo cha kugawa hard drive katika sehemu mbalimbali. Kitendo hiki husaidia kutenganisha sehemu ya ha… Read More
  • Jinsi ya Kutatua Tatizo la Barua Pepe Kutoingia Katika InboxHabari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Barua pepe ni njia ambayo watumiaji wa kompyuta hutumia kutuma ujumbe kwa njia ya kidigitali. Kuna kampuni za aina mbalimbali ambazo… Read More
  • Je, Unafahamu Kifaa Kinachoitwa Mouse? Habari rafiki, Kompyuta huundwa na vifaa vilivyogawanyika katika makundi makuu matatu. Makundi haya yamewekwa kutegemeana na kazi zinazotekelezwa na vifaa vinavyoundwa kundi husika. 1. Kundi la kwanza linajumuisha vi… Read More
  • Hatua Nne (04) Katika Uandishi wa Blogu Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki unapoanza kuandika makala katika blogu kuna changamoto mbalimbali ambazo utakutana nazo. Changamoto hizi zinatokana na kuwa … Read More

0 comments:

Post a Comment