Sunday, 13 November 2016

Namna ya Kutambua Dalili Za Kushindwa

Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio!
Rafiki gari linapopelekwa kwa fundi kwa ajili ya kutatua tatizo lililo nalo, litaweza kutatuliwa ikiwa tuu kisababishi cha tatizo husika kimefahamika . Ila pia ukienda kwa daktari wa binadamu ukiwa dhaifu , ataweza kukupatia matibabu sahihi baada ya kugundua dalili za tatizo husika. 



Kwa upande mwingine katika maisha yetu unaweza kuwa unashindwa katika kila kitu unachofanya na ukakosa mtu wa kukusaidia kuvuka hiyo hali kwa sababu tuu ya kutoa visingizio (excuse) au sababu zilizokusababishwa ushindwe.
Mambo haya yanaweza kuwa yanaumiza lakini ni bora na sahihi kufahamu ukweli ambao umekuwa hujui na namna ambavyo unaathiri fursa yako ya kufanikiwa.
Soma Makala Hii Inayohusiana : Jinsi Ya Kuishinda Hofu Uliyonayo
Kufanya jambo chini ya uwezo ulionao au kufanya tofauti na mpango uliokuwa umejiwekea ni moja ya dalili itakayokupelekea. kushindwa. Hali hii inachangiwa sawa na kujidanganya kwa kukubali maoni ya marafiki au mambo ambayo umeshafanikiwa kuyapata.
Ili kuweza kuepuka hali hii hakikisha unafanya jambo lolote kwa uwezo wako wote na kuzingatia mpango uliouweka katika kufanikisha jambo husika.
Kufanya jambo kana kwamba una muda wa miaka elfu ya kuishi ni dalili nyingine itakayokupelekea kushindwa. Na hapa utakuta kwa chochote unachofanya utakuta unafanya kama vile unayo masaa yakutosha au wakati mwingine unatumia muda wako muhimu katika mambo muhimu bila kujali kuwa muda upo na ukomo.
Ili kuweza kuepuka hali hii hakikisha unatumia muda wako vizuri kwa kuchagua kufanya yale mambo muhimu ambayo yatachangia katika kukusogeza hatua ya kutimiza malengo yako, na epuka kufanya mambo yasiyo ya msingi.
Kukubali kuchukua jambo ambalo unajua linazidi uwezo wako wa kulitenda ni dalili nyingine itakayokupelekea kushindwa. Sababu ujuzi na maarifa uliyonayo hayakidhi uwezo wa kulibeba jambo. Hivyo hata kama utalichukua ujue utafanya chini ya kiwango au utafanya bila mafanikio.
Ili kuweza kuepuka hali hii ikiwa umechukua jambo linalozidi uwezo wako hakikisha una mpango mkakati wa kukuwezesha kupandisha uwezo wako wa kimaarifa na kiujuzi utakaoweza kuhimili ukubwa wa jambo unapokwenda.
Rafiki unaweza kuwashirikisha wengine kuhusu blogu hii kwa ajili ya kupata maarifa mbalimbali na pia unaweza kubofya hapa ili kuweza kupata makala kila inapowekwa kupitia barua pepe yako.
Goodluck Moshi
Author
StadizaMafanikio

Related Posts:

  • Uchambuzi wa Kitabu " TOUGH TIMES NEVER LAST BUT TOUGH PEOPLE DO" Robert H Schuller ni mwandishi wa kitabu cha "TOUGH TIMES NEVER LAST BUT TOUGH PEOPLE DO" . Katika kitabu hiki mwandishi anatupa mbinu za kutumia tunapokuwa tunapitia vipindi vigumu katika maisha yetu ya kila siku. Hapa nina… Read More
  • Jinsi ya Kutengeneza Bootable USB Drive Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Flash ni kifaa ambacho hutumika kwa ajili ya kuhifadhi data kutoka katika kompyuta. Flash inaweza kuchomekwa na kutolewa katika kom… Read More
  • Hatua Nne (04) Katika Uandishi wa Blogu Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki unapoanza kuandika makala katika blogu kuna changamoto mbalimbali ambazo utakutana nazo. Changamoto hizi zinatokana na kuwa … Read More
  • Mfumo Pekee Utakakokusaidia Kukidhi Mahitaji ya Mteja Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Suala la kukidhi mahitaji ya mteja unaowahudumia linakwenda sambamba na utoaji wa huduma bora kwa mteja. Kiwango cha kukidhi mahita… Read More
  • Matumizi Bora ya Siku za Wikiendi na Sikukuu Habari rafiki yangu ambaye ni mfuatiliaji wa makala katika blogu hii ya Stadi za Mafanikio! Rafiki katika wiki tuna siku saba, kati ya siku hizi kuna baadhi ya watu kutegemea na ratiba ya majukumu pale anapofanya kazi anaku… Read More

0 comments:

Post a Comment